ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - فهرس التراجم


ترجمة معاني آية: (282) سورة: البقرة
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَدَايَنتُم بِدَيۡنٍ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى فَٱكۡتُبُوهُۚ وَلۡيَكۡتُب بَّيۡنَكُمۡ كَاتِبُۢ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَلَا يَأۡبَ كَاتِبٌ أَن يَكۡتُبَ كَمَا عَلَّمَهُ ٱللَّهُۚ فَلۡيَكۡتُبۡ وَلۡيُمۡلِلِ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ وَلۡيَتَّقِ ٱللَّهَ رَبَّهُۥ وَلَا يَبۡخَسۡ مِنۡهُ شَيۡـٔٗاۚ فَإِن كَانَ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ سَفِيهًا أَوۡ ضَعِيفًا أَوۡ لَا يَسۡتَطِيعُ أَن يُمِلَّ هُوَ فَلۡيُمۡلِلۡ وَلِيُّهُۥ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَٱسۡتَشۡهِدُواْ شَهِيدَيۡنِ مِن رِّجَالِكُمۡۖ فَإِن لَّمۡ يَكُونَا رَجُلَيۡنِ فَرَجُلٞ وَٱمۡرَأَتَانِ مِمَّن تَرۡضَوۡنَ مِنَ ٱلشُّهَدَآءِ أَن تَضِلَّ إِحۡدَىٰهُمَا فَتُذَكِّرَ إِحۡدَىٰهُمَا ٱلۡأُخۡرَىٰۚ وَلَا يَأۡبَ ٱلشُّهَدَآءُ إِذَا مَا دُعُواْۚ وَلَا تَسۡـَٔمُوٓاْ أَن تَكۡتُبُوهُ صَغِيرًا أَوۡ كَبِيرًا إِلَىٰٓ أَجَلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ أَقۡسَطُ عِندَ ٱللَّهِ وَأَقۡوَمُ لِلشَّهَٰدَةِ وَأَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَرۡتَابُوٓاْ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً حَاضِرَةٗ تُدِيرُونَهَا بَيۡنَكُمۡ فَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَلَّا تَكۡتُبُوهَاۗ وَأَشۡهِدُوٓاْ إِذَا تَبَايَعۡتُمۡۚ وَلَا يُضَآرَّ كَاتِبٞ وَلَا شَهِيدٞۚ وَإِن تَفۡعَلُواْ فَإِنَّهُۥ فُسُوقُۢ بِكُمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ وَيُعَلِّمُكُمُ ٱللَّهُۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na mkamfuata Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, mkiamiliana kwa mkopo mpaka muda maalumu, usajilini kwa maandishi ili kuhifadhi mali na kuondoa ugomvi. Na asimame kuandika mtu muaminifu mwenye kudhibiti. Na asilikatae hilo yule mtu aliyetunukiwa na Mwenyezi Mungu ujuzi wa uandishi. Na asimame mdaiwa kufanya imla ya deni iliyo juu yake. Na amchunge Mola wake na asipunguze chochote katika deni iliyo juu yake. Iwapo mdaiwa amezuiwa matumizi kwa ubadhirifu wake na utumiaji wake unaopita kiasi, au akawa ni mdogo au ni mwendawazimu, au hawezi kusema kwa ububu au kwa ulemavu wa kutoweza kusema kabisa, basi na asimamie shughuli ya kufanya imla msimamizi wa mdaiwa kwa niaba yake. Na takeni ushahidi wa Waislamu wawili wanaume, waliobaleghe, wenye akili na waadilifu. Iwapo hawatopatikana wanaume wawili, takeni ushahidi wa mwanamume mmoja na wanawake wawili mnaoridhika na ushahidi wao, ili akisahau mmoja wao (hao wanawake wawili) yule mwengine amkumbushe. Na ni juu ya mashahidi kukubali mwito wa mwenye kuwaita kutoa ushahidi. Na ni juu yao kutoa ushahidi wao wakitakiwa kufanya hivyo. Na msichoke kuisajili deni, iwe ni kubwa au ni ndogo, mpaka wakati wake maalumu wa kulipa. Kwani hilo ni la usawa zaidi katika Sheria ya Mwenyezi Mungu na uongofu Wake, na linasaidia sana kabisa katika kusimamisha ushahidi na kuutekeleza, na liko karibu zaidi na kuondoa shaka kuhusu deni yenyewe, kiasi chake na muda wake. Lakini, iwapo ni jambo la kuuza na kununua, kwa kuchukua bidhaa na kutoa thamani yake papo hapo, basi hakuna haja ya kusajili, na inapendekezwa kushuhudisha hilo ili kuepusha ugomvi na utesi. Na katika mambo ya lazima kwa shahidi na mwandishi ni kutekeleza ushahidi kwa njia zake na usajili kama Alvyoamrisha Mwenyezi Mungu. Na hafai kwa mwenye haki na kwa yule ambaye haki iko juu ya shingo yake kuwadhuru waandishi na mashahidi. Pia, haifai kwa waandishi na mashahidi kuwadhuru wanaohitajia uandishi wao na ushahidi wao. Na mkifanya mliyokatazwa, huko ni kutoka nje ya twaa ya Mwenyezi Mungu; na mwisho mbaya wa kitendo hiko utawafikia. Na muogopeni Mwenyezi Mungu katika maamrisho Yake yote aliyowaamrisha nayo na akawakataza nayo. Na Mwenyezi Mungu Anawajulisha yote yanayotengeneza ulimwengu wenu na Akhera yenu. Na Mwenyezi Mungu kwa kila jambo ni Mjuzi. Hakuna kitu chochote kinachofichika Kwake kuhusu mambo yenu, na Atawalipa kwa hayo.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (282) سورة: البقرة
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

إغلاق