ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - فهرس التراجم


ترجمة معاني سورة: الجمعة   آية:

سورة الجمعة - Surat Al-Jumu'ah

يُسَبِّحُ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ ٱلۡمَلِكِ ٱلۡقُدُّوسِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ
Vinamtakasa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka vyote vilivyo mbinguni na vyote vilivyo Ardhini, na Yeye Peke Yake Ndiye mfalme wa kila kitu, Aliye Mshindi kwenye utawala Wake bila ya mpinzani, Mwingi wa hekima katika kuyapelekesha mambo Yake na utengenezaji Wake.
التفاسير العربية:
هُوَ ٱلَّذِي بَعَثَ فِي ٱلۡأُمِّيِّـۧنَ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِهِۦ وَيُزَكِّيهِمۡ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَإِن كَانُواْ مِن قَبۡلُ لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Mwenyezi Munu, kutakasika na kila upungufu ni Kwake, Ndiye Aliyetuma kwa Waarabu, wasiojua kusoma wala kuwa na kitabu wala kumbukumbu zozote za utume, Mtume anayetokamana na wao aliyetumwa kwa watu wote, awasomee Qur’ani na awatakase wao na itikadi mbovu na tabia mbaya, na awafundishe wao Qur’ani na Sunnah. Na wao, kwa kweli, tangu alipokuwa hajatumilizwa, walikuwa kwenye ukengeukaji ulio waziwazi kwa kuwa kando na haki. Na Mwenyezi Mungu, kutakasika na kila upungufu ni Kwake,
التفاسير العربية:
وَءَاخَرِينَ مِنۡهُمۡ لَمَّا يَلۡحَقُواْ بِهِمۡۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Amemtuma yeye kwa watu wengine watakaokuja ambao bado hawajakuja miongoni mwa Waarabu na wengineo. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Peke Yake, Ndiye Mshindi mwenye kushinda juu ya kila kitu, Mwingi wa hekima katika maneno Yake na matendo Yake.
التفاسير العربية:
ذَٰلِكَ فَضۡلُ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ
Kutumilizwa huko kwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa ummah wa Kiarabu na wasiokuwa wao, ni wema kutoka kwa Mwenyezi Mungu humpa Anayemtaka miongoni mwa waja Wake. Na Yeye, Peke Yake, Ndiye Mwenye wema na upaji mwingi.
التفاسير العربية:
مَثَلُ ٱلَّذِينَ حُمِّلُواْ ٱلتَّوۡرَىٰةَ ثُمَّ لَمۡ يَحۡمِلُوهَا كَمَثَلِ ٱلۡحِمَارِ يَحۡمِلُ أَسۡفَارَۢاۚ بِئۡسَ مَثَلُ ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Mfano wa Mayahudi ambao walitakiwa kuifuata Taurati kivitendo kisha wakakosa kuifuata ni kama mfano wa punda ambaye yuwabeba vitabu na hajui yaliyo ndani yake. Ni mfano muovu mno wa watu ambao wamezikataa aya za Mwenyezi Mungu na wasifaidike nazo. Na Mwenyezi mungu Hawaelekezi kwenye wema watu madhalimu ambao wanaikiuka mipaka Yake na wanaotoka nje ya utiifu Kwake.
التفاسير العربية:
قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ هَادُوٓاْ إِن زَعَمۡتُمۡ أَنَّكُمۡ أَوۡلِيَآءُ لِلَّهِ مِن دُونِ ٱلنَّاسِ فَتَمَنَّوُاْ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Sema, ewe Mtume, uwaambie wale ambao wameshikamana na desturi za kiyahudi zilizopotoka, «Mkidai kiurongo kwamba nyinyi tu ndio vipenzi vya Mwenyezi Mungu na sio watu wengine, basi tamanini kufa iwapo nyinyi ni wakweli katika madai yenu kuwa Mwenyezi Mungu Anawapenda nyinyi.»
التفاسير العربية:
وَلَا يَتَمَنَّوۡنَهُۥٓ أَبَدَۢا بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّٰلِمِينَ
Na wala hawa Mayahudi hawatatamani kifo kabisa kwa vile wanavyoyapenda maisha ya duniani kuliko Akhera na kwa kuogopa kuteswa na Mwenyezi Mungu kwa sababu ya yale waliyoyatanguliza ya ukafiri na matendo maovu. Na Mwenyezi Mungu Anawajua mno madhalimu, hakifichamani Kwake chochote cha udhalimu wao.
التفاسير العربية:
قُلۡ إِنَّ ٱلۡمَوۡتَ ٱلَّذِي تَفِرُّونَ مِنۡهُ فَإِنَّهُۥ مُلَٰقِيكُمۡۖ ثُمَّ تُرَدُّونَ إِلَىٰ عَٰلِمِ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Sema, «Kwa kweli mauti mnayoyakimbia hayakimbiliki, kwani ni yenye kuwajia wakati wenu wa kufa utakapofika, kisha Siku ya kufufuliwa mtarudishwa kwa Mwenyezi Mungu mjuzi wa yale yaliyofichamana na yanayoonekana, na hapo Atawapasha habari ya matendo yenu na Atawalipa nyinyi kwa hayo.»
التفاسير العربية:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَوٰةِ مِن يَوۡمِ ٱلۡجُمُعَةِ فَٱسۡعَوۡاْ إِلَىٰ ذِكۡرِ ٱللَّهِ وَذَرُواْ ٱلۡبَيۡعَۚ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo! Pindi mwadhini atakapoita kwa ajili ya Swala Siku ya Ijumaa, endeni upesi msikilize hutuba na mtekeleze Swala, na muache uuzaji na pia ununuaji na kila kinachowashughulisha nyinyi na hiyo Swala. Hilo mliloamrishwa ni bora kwenu nyinyi kutokana na yaliyo humo ya kusamehewa dhambi zenu na kupatiwa malipo mema kutoka kwa Mwenyezi Mungu.Basi iwapo nyinyi mnayajua manufaa ya nafsi zenu, fanyeni hilo. Kwenye aya hii kuna dalili kwamba kwenda kuhudhuria Swala ya Ijumaa na kusikiliza hutuba ni lazima.
التفاسير العربية:
فَإِذَا قُضِيَتِ ٱلصَّلَوٰةُ فَٱنتَشِرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَٱبۡتَغُواْ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ وَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا لَّعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Basi mkisha kuisikia hutuba na mkaitekeleza Swala, tawanyikeni kwenye ardhi na mtafute riziki ya Mwenyezi Mungu kwa kwenda mbio kwenu, na mtajeni Mwenyezi Mungu kwa wingi katika hali zenu zote, ili mfaulu kuzipata kheri mbili: za duniani na za Akhera.
التفاسير العربية:
وَإِذَا رَأَوۡاْ تِجَٰرَةً أَوۡ لَهۡوًا ٱنفَضُّوٓاْ إِلَيۡهَا وَتَرَكُوكَ قَآئِمٗاۚ قُلۡ مَا عِندَ ٱللَّهِ خَيۡرٞ مِّنَ ٱللَّهۡوِ وَمِنَ ٱلتِّجَٰرَةِۚ وَٱللَّهُ خَيۡرُ ٱلرَّٰزِقِينَ
Na pindi wanapoona baadhi ya Waislamu biashara au chochote miongoni mwa viliwazo vya duniani na pambo lake, hutawanyika kwenda huko na wakakuacha wewe umesimama juu ya mimbari unatoa hutuba. Waambie, ewe Nabii, «Yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ya thawabu na neema yana manufaa zaidi kwenu kuliko pumbao na biashara. Na Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Ndiye Bora wa wanaoruzuku na kutoa, basi muombeni na mjisaidie kwa kumtii, ili myapate yaliyoko Kwake ya kheri mbili: ya duniani na ya Akhera.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: الجمعة
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

إغلاق