ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (116) سورة: هود
فَلَوۡلَا كَانَ مِنَ ٱلۡقُرُونِ مِن قَبۡلِكُمۡ أُوْلُواْ بَقِيَّةٖ يَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡفَسَادِ فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا قَلِيلٗا مِّمَّنۡ أَنجَيۡنَا مِنۡهُمۡۗ وَٱتَّبَعَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَآ أُتۡرِفُواْ فِيهِ وَكَانُواْ مُجۡرِمِينَ
Basi mbona hawakuwamo katika watu wa kabla yenu wenye vyeo na wasaa wanao kataza uharibifu katika nchi, isipo kuwa wachache tu, ambao ndio tulio waokoa? Na walio dhulumu walifuata starehe zao, na wakawa ni wakosefu.
Ilikuwa inapasa katika kaumu zilizo tangulia na tukaziteketeza kwa dhulma zao, wawepo jamaa kati yao wenye kusikilizwa kauli yao, na wenye vyeo katika dini na akili, wawakanye wenzi wao waache uharibifu katika nchi, ili wasalimike na adhabu iliyo wateremkia. Lakini hayakuwa hayo. Yaliyo tokea ni kuwa walikuwapo Waumini wachache wasio sikilizwa rai zao wala uwongozi wao. Hao Mwenyezi Mungu aliwaokoa pamoja na Mitume wao wakati ule walipo shikilia wenye kudhulumu wenye inda kung'ang'anilia yale maisha ya anasa na fisadi waliyo yazoea. Hayo yakawa ni pingamizi wasiweze kunafiika na wito wa Haki na kheri, na kwa kukhiari kwao njia hiyo wakazama katika madhambi na vitendo viovu. Basi Mwenyezi Mungu akawahiliki kwa mujibu wa mwendo wake wa maumbile.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (116) سورة: هود
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق