ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (31) سورة: يوسف
فَلَمَّا سَمِعَتۡ بِمَكۡرِهِنَّ أَرۡسَلَتۡ إِلَيۡهِنَّ وَأَعۡتَدَتۡ لَهُنَّ مُتَّكَـٔٗا وَءَاتَتۡ كُلَّ وَٰحِدَةٖ مِّنۡهُنَّ سِكِّينٗا وَقَالَتِ ٱخۡرُجۡ عَلَيۡهِنَّۖ فَلَمَّا رَأَيۡنَهُۥٓ أَكۡبَرۡنَهُۥ وَقَطَّعۡنَ أَيۡدِيَهُنَّ وَقُلۡنَ حَٰشَ لِلَّهِ مَا هَٰذَا بَشَرًا إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا مَلَكٞ كَرِيمٞ
Alipo sikia yule bibi masengenyo yao aliwaita, na akawawekea matakia ya kuegemea, na akampa kila mmoja wao kisu. Akamwambia Yusuf: Tokeza mbele yao. Basi walipo mwona waliona ni kitu kikubwa kabisa, na wakajikata mikono yao. Wakasema: Hasha Lillahi! Huyu si mwanaadamu. Hakuwa huyu ila ni Malaika mtukufu.
Yule bibi alipo yasikia masengenyo yao wale wanawake na kuwa wanamsema kwa vibaya, aliwaalika nyumbani kwake na akawapangia matakia na mito ya kuegemea, na akampa kila mmoja wao kisu, baada ya kwisha hudhuria na wakakaa wakiegemea. Akawaletea chakula na visu vya kulia. Akamwambia Yusuf: Hebu watokee! Alipotokeza wakamwona walistaajabu. Uzuri wake ulio pita mpaka uliwatwaa wasijitambue, wakawa wanajikata mikono yao jinsi ya kushtuka kwao, na huku wanadhani wanakata chakula! Wakasema kwa mastaajabu na kushituka: Hasha Lillahi! Mungu apishe mbali! Huyu tunaye mwona si binaadamu! Hapana binaadamu mwenye uzuri namna hii, na mwenye jamali kama hivi, na usafi kama huu, na kunyooka kama huku! Huyu ni Malaika tu, mwenye uzuri huu, na sifa hizi zilio timia!
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (31) سورة: يوسف
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق