ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (36) سورة: النحل
وَلَقَدۡ بَعَثۡنَا فِي كُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولًا أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱجۡتَنِبُواْ ٱلطَّٰغُوتَۖ فَمِنۡهُم مَّنۡ هَدَى ٱللَّهُ وَمِنۡهُم مَّنۡ حَقَّتۡ عَلَيۡهِ ٱلضَّلَٰلَةُۚ فَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani. Basi kati yao wapo alio waongoa MwenyeziMungu. Na kati yao wapo ambao ulio wathibitikia upotovu. Basi tembeeni katika ardhi, muangalie ulikuwaje mwisho wa wanao kanusha.
Na kila umma tuliwapelekea Mtume awaambie: Muabuduni Mwenyezi Mungu peke yake. Na jitengeni na kila jabari mharibifu. Na wafikishie ujumbe, na uwaongoze. Basi kikundi kikasikiliza uwongozi na kikafuata, na Mwenyezi Mungu akakiongoa kwa kuwa kilijitayarisha vizuri kufuata Njia Iliyo Nyooka. Na kikundi kingine kikapuuza kusikia Haki, kikastahiki kwenda njia potovu, na Mwenyezi Mungu akakipelekea adhabu. Na ikiwa nyinyi, washirikina wa Makka, mna shaka na haya, basi tembeeni katika nchi za karibu nanyi, muangalie, mzingatie nini kilicho washukia wanao kanusha, kina A'ad na Thamud na Kaumu Luut'i. Na vipi ilikuwa khasara yao na hilaki yao katika mwisho wao!
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (36) سورة: النحل
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق