ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (96) سورة: البقرة
وَلَتَجِدَنَّهُمۡ أَحۡرَصَ ٱلنَّاسِ عَلَىٰ حَيَوٰةٖ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْۚ يَوَدُّ أَحَدُهُمۡ لَوۡ يُعَمَّرُ أَلۡفَ سَنَةٖ وَمَا هُوَ بِمُزَحۡزِحِهِۦ مِنَ ٱلۡعَذَابِ أَن يُعَمَّرَۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ
Na hakika utawaona ni wenye kuwashinda watu wote kwa pupa ya kuishi, na kuliko washirikina. Kila mmoja wao anatamani lau angeli pewa umri wa miaka elfu. Wala hayo ya kuzidishiwa umri hayamuondoshei adhabu; na Mwenyezi Mungu anayaona wanayo yatenda.
Bila ya shaka yoyote utawakuta wao ndio wamewashinda watu wote kwa pupa waliyo nayo kuwania maisha ya dunia ya kila namna, ya utukufu na unyonge. Na hiyo pupa yao inashinda ya makafiri washirikina (mapagani) wasio amini kufufuliwa wala Pepo. Kwa hivyo wanapenda lau kuwa wangelizidishiwa umri wakaishi hata miaka elfu. Na hata wangeliishi vipi hawawezi kuepuka adhabu ya Mwenyezi Mungu inayo wangojea. Kwani Yeye ni Mjuzi wa hao madhaalimu, na atawaonjesha malipo ya vitendo vyao wanavyo vitenda
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (96) سورة: البقرة
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق