ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (78) سورة: الأنبياء
وَدَاوُۥدَ وَسُلَيۡمَٰنَ إِذۡ يَحۡكُمَانِ فِي ٱلۡحَرۡثِ إِذۡ نَفَشَتۡ فِيهِ غَنَمُ ٱلۡقَوۡمِ وَكُنَّا لِحُكۡمِهِمۡ شَٰهِدِينَ
Na Daud na Suleiman walipo kata hukumu katika kadhiya ya konde walipo lisha humo mbuzi wa watu usiku. Na Sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao hiyo.
Ewe Nabii! Wataje Daud na Suleiman walipo toa hukumu katika kesi ya konde, ilio ingiliwa na mbuzi wa watu mbali usiku na wakala mazao yake. Na Sisi tulikuwa tunaijua hukumu iliyo khusiana na kesi hiyo. Kisa cha hiyo hukumu: Mbuzi waliingia usiku mmoja katika konde ya mtu, wasibakishe kitu. Daud akahukumu kuwa wale mbuzi wawe wa mwenye konde kulipia khasara yake. Suleiman akatoa hukumu nyengine, akasema: Mbuzi wale wabakie mkononi mwa mwenye konde mpaka itapo mea tena mazao yake, na avumilie kwa yaliyo mpata. Na baada yake warejesheane.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (78) سورة: الأنبياء
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق