ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (45) سورة: آل عمران
إِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكِ بِكَلِمَةٖ مِّنۡهُ ٱسۡمُهُ ٱلۡمَسِيحُ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ وَجِيهٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).
Kumbuka na utaje ewe Nabii, pale Malaika walipo mbashiria Maryamu kuwa atamzaa mwana kwa neno lake tu Mwenyezi Mungu kinyume na ada wanavyo zaliwa watu. Jina lake mwana huyo ni Masihi Isa bin Maryamu. Na Mwenyezi Mungu amemjaalia hapa duniani kuwa atakuwa na cheo kwa unabii wake na kuepukana na aibu zote, na kesho Akhera kuwa atakuwa na cheo cha juu pamoja na kundi la walio takasika, wakawa wenye kuwa karibu mno na Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii walio imara baraabara.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (45) سورة: آل عمران
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق