ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (93) سورة: آل عمران
۞ كُلُّ ٱلطَّعَامِ كَانَ حِلّٗا لِّبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ إِلَّا مَا حَرَّمَ إِسۡرَٰٓءِيلُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ مِن قَبۡلِ أَن تُنَزَّلَ ٱلتَّوۡرَىٰةُۚ قُلۡ فَأۡتُواْ بِٱلتَّوۡرَىٰةِ فَٱتۡلُوهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israili isipo kuwa alicho jizuilia Israili mwenyewe kabla haijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome ikiwa nyinyi ni wasema kweli.
Mayahudi waliwatoa kombo Waislamu kwa kuhalalisha baadhi ya vyakula kama nyama ya ngamia na maziwa yake. Wakadai kuwa hayo yaliharimishwa na sharia ya Ibrahim. Mwenyezi Mungu Subhanahu aliwarudi madai yao hayo kwa kubainisha kuwa vyakula vyote vilikuwa halali kwa Wana wa Yaakub (ndiye Israil) kabla ya kuteremka Taurati, ila alicho jizuia Yaakub mwenyewe kwa sababu zilizo mkhusu yeye tu, basi na wao wakijiharimishia nafsi zao. Mwenyezi Mungu akamuamrisha Nabii wake awatake walete uthibitisho wa Taurati kuwa sharia ya Ibrahim imeharimisha hayo kama wao wanasema kweli. Wakashindwa, wakanywea.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (93) سورة: آل عمران
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق