ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (176) سورة: النساء
يَسۡتَفۡتُونَكَ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِي ٱلۡكَلَٰلَةِۚ إِنِ ٱمۡرُؤٌاْ هَلَكَ لَيۡسَ لَهُۥ وَلَدٞ وَلَهُۥٓ أُخۡتٞ فَلَهَا نِصۡفُ مَا تَرَكَۚ وَهُوَ يَرِثُهَآ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهَا وَلَدٞۚ فَإِن كَانَتَا ٱثۡنَتَيۡنِ فَلَهُمَا ٱلثُّلُثَانِ مِمَّا تَرَكَۚ وَإِن كَانُوٓاْ إِخۡوَةٗ رِّجَالٗا وَنِسَآءٗ فَلِلذَّكَرِ مِثۡلُ حَظِّ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۗ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمۡ أَن تَضِلُّواْۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمُۢ
Wanakuomba uhukumu, sema: Mwenyezi Mungu anakupeni hukumu juu ya mkiwa. Ikiwa mtu amekufa, naye hana mtoto, lakini anaye ndugu wa kike, basi huyo atapata nusu alicho acha maiti. Na mwanamume atamrithi ndugu wa kike ikiwa hana mwana. Na ikiwa wao ni ndugu wa kike wawili, basi watapata thuluthi mbili za alicho acha maiti. Na wakiwa ndugu wanaume na wanawake, basi mwanamume atapata sehemu iliyo sawa na ya wanawake wawili. Mwenyezi Mungu anakubainishieni ili msipotee; na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Ewe Nabii! Wanakuuliza vipi atarithiwa aliye kufa naye akawa hana mwana, wala mzazi. Sema: Hakika hukumu ya Mwenyezi Mungu katika urithi wa hawa ni kuwa, akiwa maiti ana ndugu wa kike basi atapata nusu ya tirka. Na akiwa maiti ni mwanamke naye ana ndugu wa kiume basi atarithi mali yote. Na ikiwa ameacha ndugu wawili wa kike, basi watapata hao thuluthi mbili ya urithi. Na ikiwa hao ndugu ni mchanganyiko wanaume na wanawake, basi fungu la mwanamume ni sawa na mafungu mawili ya wanawake. Mwenyezi Mungu anakubainishieni haya msije mkapotea katika kugawa mafungu ya urithi. Na Mwenyezi Mungu ni Mkamilifu wa ujuzi wa a'mali zenu na vitendo vyenu vyote. Na atakulipeni kwavyo. (Angalia: Urithi wa ndugu katika Aya hii ni wa ndugu khalisa, yaani ndugu kwa baba na mama, au ndugu kwa baba. Ama urithi wa ndugu kwa mama tu umekwisha tajwa katika Aya 12 ya Sura hii ya Annisaa.) Na Sunna (Mafunzo ya Mtume) imebainisha kuwa wakizidi kuliko ndugu wa kike wawili, pamoja na Aya ya mirathi iliyo tajwa, kuwa wakizidi kuliko binti wawili, watachukua thuluthi mbili. Ni bora kuwa zaidi kuliko ndugu wawili wa kike, kwa sababu mabinti ni karibu zaidi kwa maiti. Tuzingatie kuwa kwa mujibu wa kanuni za Kizungu za kurithi, ambazo zimetokana na kanuni ya Kirumi, ndugu wanaume wala wa kike wala watoto wao hawarithi. Na juu ya hivyo mwenye mali anayo ruhusa kumkata yeyote asipate urithi wake. Uislamu umekataza haya. Warithi lazima wapate urithi wao, ila mtu anayo haki ya kuandika wasia kujihukumia kisicho zidi thuluthi moja ya mali yake.(W.H. Ingrams katika kitabu chake Zanzibar Its History and Its People ameandika: "Hakika Sharia Takatifu yaonekana kuwa ni ya haki zaidi sana kuliko hata mpango wa Kiingereza wa kugawanya mali. Katika Zanzibar [na bila ya shaka katika Waislamu wote] hapana mwendo wa kuwa mtu "kukatwa urithi akabakishwa na shilingi moja tu"; vyo vyote vile, ni sehemu ndogo tu ndiyo inaweza kuandikiwa wasia, na yaliyo baki lazima yagawiwe kwa warithi kwa mujibu wa kiwango maalumu.")
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (176) سورة: النساء
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق