Hayo ndiyo aliyo wabashiria Mwenyezi Mungu waja wake walio amini na wakatenda mema. Sema: Sikuombeni malipo yoyote kwenu ila mapenzi katika kujikurubisha. Na anaye fanya wema tutamzidishia wema. Hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehevu Mwenye shukrani.
Hiyo fadhila kubwa ndiyo ambayo Mwenyezi Mungu amewabashiria waja wake Waumini, wat'iifu. Ewe Mtume! Sema: Mimi sitaki kwenu ujira kwa kufikisha huu Ujumbe, isipo kuwa mumpende Mwenyezi Mungu na Mtume wake katika kujikurubisha kwenu kwake Yeye Subhanahu, kwa vitendo vyema. Na mwenye kutenda ut'iifu Mwenyezi Mungu atampa ujira mara mbili. Hakika Mwenyezi Mungu ni mkunjufu wa maghfira kwa wenye madhambi, ni Mwenye shukrani kwa waja wake wenye vitendo vyema.
Ati wanasema: Amemzulia Mwenyezi Mungu uwongo? Mwenyezi Mungu akipenda atapiga muhuri juu ya moyo wako. Na Mwenyezi Mungu anaufuta upotofu na anaithibitisha Haki kwa maneno yake. Hakika Yeye anayajua yaliomo vifuani.
Je! makafiri wanasema Muhammad anamzulia uwongo Mwenyezi Mungu? Mwenyezi Mungu akipenda atakufungia moyo wako usubiri maudhi yao, na tuhuma yao kuwa unamzulia Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ataondoa na ataushinda ukafiri na ataupa nguvu Uislamu na ataudhihirisha kwa wa'hyi alio mteremshia Mtume wake s.a.w., kwani - Yeye- Mwenyezi Mungu anajua yote yaliomo ndani ya nyoyo zenu nyote.
Naye ndiye anaye pokea toba kwa waja wake, na anasamehe makosa, na anayajua mnayo yatenda.
Ni Mwenyezi Mungu peke yake ndiye Mwenye kupokea toba kwa watu wanao mt'ii hata kwa makosa yaliyo zaidi kuliko yale wanayo ombea toba. Na Yeye ndiye anaye samehe madhambi yote isipo kuwa shirki, kwa kufadhili na kurehemu; na anayajua myatendayo ikiwa ya kheri au shari.
Na anawaitikia wanao amini na wakatenda mema, na anawazidishia fadhila zake. Na makafiri watakuwa na adhabu chungu.
Na huwaitikia Waumini kwa wanayo yaomba, na huwazidishia juu ya hayo wanayo yaomba. Na makafiri watapata adhabu yenye kufikia ukomo wa ukali na uchungu.
Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli wakunjulia riziki waja wake, basi bila ya shaka wangeli panda kiburi katika dunia. Lakini anaiteremsha kwa kipimo akitakacho. Hakika Yeye anawajua vyema waja wake na anawaona.
Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli wakunjulia waja wake wote, kama watakavyo, basi bila ya shaka wangeli panda kiburi katika ardhi wakafanya dhulma. Lakini Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye, na humdhikisha amtakaye, kwa mujibu wa hikima yake. Hakika Mwenyezi Mungu anayajua vyema mambo yote ya waja wake, ya siri na dhaahiri. Basi Yeye humkadiria kila mmoja kwa linalo msilihi kwa mujibu wa hikima yake.
Naye ndiye anaye iteremsha mvua baada ya wao kwisha kata tamaa, na hueneza rehema yake. Naye ndiye Mlinzi Mwenye kuhimidiwa.
Na Mwenyezi Mungu, peke yake, ndiye anaye iteremsha mvua inayo waokoa na ukame baada ya kwisha kata tamaa na kuzidi kiangazi, kuwa ni rehema kwa waja wake. Na Yeye hueneza baraka za mvua katika mimea, na miti ya matunda, na wanyama, na nyanda, na milima. Na Yeye, peke yake, ndiye Mwenye madaraka ya kuyapanga mambo yote ya waja wake, na ndiye wa kuhimidiwa kwa neema zake, na vitendo vyake vyote.
Na katika Ishara zake ni kuumba mbingu na ardhi, na wanyama alio waeneza. Naye ni Mwenye uweza wa kuwakusanya apendapo.
Na katika dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu kuumba atakacho ni huku kuumba mbingu na ardhi kwa nidhamu iliyo pangwa; na kuumbwa vilivyo tenganishwa humo na kuenezwa wanayama wanao onekana na wengineo. Na Mwenyezi Mungu aliye hakikisha uweza wake kwa kuumba hivyo vilio tajwa ni Muweza wa kuwakusanya wote katika wakati autakao kuwafufulia kwa ajili ya malipo.
Na misiba inayo kusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi.
Na msiba wowote unao kusibuni mnao uchukia ni kwa sababu ya maasi yenu. Na anayo yasamehe Mwenyezi Mungu duniani au akayachukulia ahadi humo, basi Mwenyezi Mungu ni Karimu; hatokuwa tena wa kuadhibu kwa hayo Akhera. Na Kwa hivi ametakasika na dhulma, na amesifika kwa rehema kunjufu.
Na nyinyi hamwezi kushinda katika ardhi. Na wala nyinyi hamna mlinzi wala msaidizi badala ya Mwenyezi Mungu.
Wala nyinyi hamwezi kumshinda Mwenyezi Mungu na kumzuilia asilete masaibu duniani kuwa ni adhabu kwa ajili ya maasi yenu, na hata mkikimbia vipi. Na wala hamna asiye kuwa Mwenyezi Mungu wa kukurehemuni pindi ikikuteremkieni balaa, wala hamna wa kukunusuruni nayo.
4. إبقاء معلومات نسخة الترجمة الموجودة داخل المستند.
5. إفادة المصدر (QuranEnc.com) بأي ملاحظة على الترجمة.
6. تطوير الترجمات وفق النسخ الجديدة الصادرة من المصدر (QuranEnc.com).
7. عدم تضمين إعلانات لا تليق بترجمات معاني القرآن الكريم عند العرض.
نتائج البحث:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".