للإطلاع على الموقع بحلته الجديدة

ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني سورة: المرسلات   آية:

سورة المرسلات - Al-Mursalat

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole! [1]
[1] Naapa kwa Aya zilizo tumwa kwa ulimi wa Jibrili kumpelekea Muhammad kwa upole wa kawaida na kheri,
التفاسير العربية:
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا
Na zinazo vuma kwa kasi! [2]
[2] Na kwa Aya zenye kuzitwaa kwa nguvu dini nyengine zote za uwongo zikizipeperushia mbali,
التفاسير العربية:
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا
Na zikaeneza maeneo yote! [3]
[3] Na kwa Aya zenye kueneza hikima na uwongofu katika nyoyo za walimwengu kwa uenezi mkubwa mno,
التفاسير العربية:
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا
Na zinazo farikisha zikatawanya! [4]
[4] Na zenye kufarikisha baina ya kweli na uwongo kwa mfarakano ulio wazi kabisa,
التفاسير العربية:
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا
Na zinazo peleka mawaidha! [5]
[5] Na zenye kuwapa watu mawaidha ya kuwanufaisha,
التفاسير العربية:
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا
Kwa kuudhuru au kuonya, [6]
[6] Ili iwe ni udhuru kwao na onyo wasiwe na hoja,
التفاسير العربية:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa! [7]
[7] Hakika haya mliyo ahidiwa ya kuja Kiyama kwa yakini yatatimia tu bila ya shaka yoyote.
التفاسير العربية:
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ
Wakati nyota zitakapo futwa, [8]
[8] Basi nyota zitapo ondolewa kabisa,
التفاسير العربية:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ
Na mbingu zitakapo pasuliwa, [9]
[9] Na mbingu zitapo pasuka,
التفاسير العربية:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ
Na milima itakapo peperushwa, [10]
[10] Na milima ikavurugwa na ikapeperushiwa mbali na upepo,
التفاسير العربية:
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao, [11]
[11] Na Mitume wakawekewa wakati maalumu wahudhurie kwa ajili ya kuwatolea ushahidi kaumu zao.
التفاسير العربية:
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo? [12]
[12] Kwa ajili ya siku gani yametayarishwa mambo haya makubwa makubwa?
التفاسير العربية:
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ
Kwa siku ya kupambanua! [13]
[13] Kwa ajili ya siku watakapo pambanuliwa baina ya viumbe.
التفاسير العربية:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini? [14]
[14] Na nini cha kukujuvya ina nini hiyo siku ya kupambanua?
التفاسير العربية:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha! [15]
[15] Ni maangamio ya milele siku hiyo kwa hao wanao kadhibisha walio waahidi Mitume!
التفاسير العربية:
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia? [16]
[16] Kwani hatukuwaangamiza mataifa ya zamani yaliyo kadhibisha,
التفاسير العربية:
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia? [17]
[17] Na kisha tukawafuatilizia hao wenginewe tukawateketeza hali kadhaalika,
التفاسير العربية:
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu! [18]
[18] Kwa madhambi waliyo yafanya na walivyo mkataa Mwenyezi Mungu?
التفاسير العربية:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [19]
[19] Siku hiyo ni siku ya kuteketezwa walio kadhibisha, kama tulivyo waahidi.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: المرسلات
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق