ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (54) سورة: الأنفال
كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَغۡرَقۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَۚ وَكُلّٞ كَانُواْ ظَٰلِمِينَ
Ni kama ada ya watu wa Firauni na walio kabla yao - walizikanusha Ishara za Mola wao Mlezi, basi tukawateketeza kwa madhambi yao. Na tukawazamisha watu wa Firauni. Na wote walikuwa wenye kudhulumu.
Kama ilivyo kuwa ada yao na mtindo wao hawa katika kuzikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu na neema zake ni kama mtindo wa watu wa Firauni na walio watangulia, hali kadhaalika ada yao na shani yao katika kuendelea kuwakadhibisha Mitume wake, na dalili za Unabii wao, ni kama ada ya watu wa Firauni na walio kabla yao. Basi wamefanana hao katika kukanusha Ishara, na kuupinga Utume wa Mitume, na kuwakadhibisha, na kuendelea juu ya mwendo huo vile vile. Na kila mmoja Mwenyezi Mungu amemtia mkononi kwa dhambi zake -wale kwa midharuba, na vimbunga, na kadhaalika; na watu wa Firauni kwa kuwazamisha. Na wote walikuwa ni madhaalimu wa nafsi zao. Kwa hivyo walistahiki adhabu iliyo wafika.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (54) سورة: الأنفال
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق