Check out the new design

Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: Yusuf   Ayə:
وَرَٰوَدَتۡهُ ٱلَّتِي هُوَ فِي بَيۡتِهَا عَن نَّفۡسِهِۦ وَغَلَّقَتِ ٱلۡأَبۡوَٰبَ وَقَالَتۡ هَيۡتَ لَكَۚ قَالَ مَعَاذَ ٱللَّهِۖ إِنَّهُۥ رَبِّيٓ أَحۡسَنَ مَثۡوَايَۖ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلظَّٰلِمُونَ
Na mke wa yule kiongozi, ambaye Yūsuf alikuwa nyumbani kwake, alimtaka Yūsuf kwa upole na kubembeleza, kwa kuwa alimpenda sana na kwa ajili ya uzuri wake, na akamfungia milango na akasema kumwambia Yūsuf, «Njoo kwangu.» Akasema, «Najilinda kwa Mwenyezi Mungu na najihifadhi Kwake na kujihami kutokana na hayo unayoniitia ya kumfanyia hiana bwanangu aliyeyafanya mazuri mashukio yangu na akanikirimu. Sitamhini kwa watu wake. Hakika hafaulu anayedhulumu na akafanya mambo ambayo hatakiwi kuyafanya.
Ərəbcə təfsirlər:
وَلَقَدۡ هَمَّتۡ بِهِۦۖ وَهَمَّ بِهَا لَوۡلَآ أَن رَّءَا بُرۡهَٰنَ رَبِّهِۦۚ كَذَٰلِكَ لِنَصۡرِفَ عَنۡهُ ٱلسُّوٓءَ وَٱلۡفَحۡشَآءَۚ إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Na nafsi yake ilivutika kufanya machafu, na Yūsuf nafsi yake ilipitiwa na mawazo ya kukubali, lau si yeye kuona alama miongoni mwa alama za Mola wake zenye kumkemea kufanya yale ambayo nafsi yake ilimzungumzia. Hakika tulimuonesha hilo, ili tumuepushiye baya na chafu katika mambo yake yote. Yeye ni miongoni mwa waja wetu waliosafishwa walioteulia kwa ujumbe na waliotakasa katika kumuabudu kwao Mwenyezi Mungu na kumpwekesha.
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱسۡتَبَقَا ٱلۡبَابَ وَقَدَّتۡ قَمِيصَهُۥ مِن دُبُرٖ وَأَلۡفَيَا سَيِّدَهَا لَدَا ٱلۡبَابِۚ قَالَتۡ مَا جَزَآءُ مَنۡ أَرَادَ بِأَهۡلِكَ سُوٓءًا إِلَّآ أَن يُسۡجَنَ أَوۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Yūsuf alikimbilia mlangoni kutaka kutoka, na yeye (mke wa kiongozi) akafanya haraka kumshika na akamvuta nguo yake kwa nyuma ili kumzuia asitoke na akaipasua. Wakamkuta mumewe kwenye mlango, hapo akasema (mke wa Kiongozi), «Ni yapi malipo ya anayetafuta jambo baya kwa mke wako, isipokuwa ni afungwe au apewe adhabu yenye uchungu?»
Ərəbcə təfsirlər:
قَالَ هِيَ رَٰوَدَتۡنِي عَن نَّفۡسِيۚ وَشَهِدَ شَاهِدٞ مِّنۡ أَهۡلِهَآ إِن كَانَ قَمِيصُهُۥ قُدَّ مِن قُبُلٖ فَصَدَقَتۡ وَهُوَ مِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Yūsuf akasema, «Yeye ndiye aliyetaka hilo kwangu. Na akatoa ushahidi mtoto wa mlezini katika jamaa zake(mke wa kiongozi) na akasema, «Iwapo kanzu yake imepasuka kwa mbele, basi mwanamke amesema kweli katika tuhma alizomfanyia na yeye (Yūsuf) ni miongoni mwa warongo.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِن كَانَ قَمِيصُهُۥ قُدَّ مِن دُبُرٖ فَكَذَبَتۡ وَهُوَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
«Na iwapo nguo yake imeraruliwa kwa nyuma , basi mwanamke amesema urongo katika kauli yake, na yeye (Yūsuf) ni miongoni mwa wakweli.»
Ərəbcə təfsirlər:
فَلَمَّا رَءَا قَمِيصَهُۥ قُدَّ مِن دُبُرٖ قَالَ إِنَّهُۥ مِن كَيۡدِكُنَّۖ إِنَّ كَيۡدَكُنَّ عَظِيمٞ
Yule mume alipoiona nguo ya Yūsuf imeraruliwa kwa nyuma alijua kwamba Yūsuf hana hatia na akasema kumwambia mke wake, «Urongo huu uliomtuhumu nao kijana huyu ni katika jumla ya vitimbi vyenu, enyi wanawake, kwani vitimbi vyenu ni vikubwa.»
Ərəbcə təfsirlər:
يُوسُفُ أَعۡرِضۡ عَنۡ هَٰذَاۚ وَٱسۡتَغۡفِرِي لِذَنۢبِكِۖ إِنَّكِ كُنتِ مِنَ ٱلۡخَاطِـِٔينَ
Akasema kiongozi wa Misri, «Ewe Yūsuf! acha kutaja mambo yaliykuwa kutoka kwake na usimwambie yoyote. Na uombe msamaha wa dhambi zako kwa Mola wako, ewe mwanamke, iwapo wewe ni miongoni mwa wale waliofanya hatia kwa kumtaka Yūsuf kimapenzi bila ya yeye kutaka na kwa kumzulia urongo.»
Ərəbcə təfsirlər:
۞ وَقَالَ نِسۡوَةٞ فِي ٱلۡمَدِينَةِ ٱمۡرَأَتُ ٱلۡعَزِيزِ تُرَٰوِدُ فَتَىٰهَا عَن نَّفۡسِهِۦۖ قَدۡ شَغَفَهَا حُبًّاۖ إِنَّا لَنَرَىٰهَا فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Habari ziliwafikia wanawake mjini wakaizungumza kuhusu hizo na wakasema kwa njia ya kumpinga mke wa kiongozi, «Mke wa Bwana anajaribu kumtaka mtumwa wake na amwita amjie. Na mapenzi yake yamefikia kwenye ngozi ya moyo wake. Hakika sisi tunamuona yeye kuwa yuko kwenye upotevu waziwazi.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: Yusuf
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. - Tərcumənin mündəricatı

Tərcümə edən: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkir və Şeyx Nasir Xamis.

Bağlamaq