Check out the new design

Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Ənbiya   Ayə:
وَٱلَّتِيٓ أَحۡصَنَتۡ فَرۡجَهَا فَنَفَخۡنَا فِيهَا مِن رُّوحِنَا وَجَعَلۡنَٰهَا وَٱبۡنَهَآ ءَايَةٗ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na kumbuka, ewe Mtume, kisa cha Maryam binti ya 'Imran aliyeihifadhi tupu yake na haramu na asifanye uzinifu katika maisha yake. Mwenyezi Mungu Akamtuma Jibrili, amani imshukiye, kwake akapuliza katika mfuko wa kanzu yake, na ule mpulizo ukafika kwenye uzao wake, na Mwenyezi Mungu akamuumba Al-Masīḥ 'Īsā, amani imshukie. Hivyo basi akabeba mimba yake bila ya mume, na kwa ajili hiyo akawa , yeye na mwanawe, ni alama ya uweza wa Mwenyezi Mungu na mazingatio kwa viumbe mpaka kusimama Kiyama.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُونِ
Manabii hawa wote, dini yao ni moja, nayo ni Uislamu. Nao ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kwa kuwa mtiifu na kumpwekesha Yeye kwa ibada. Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Ndiye Bwana wa viumbe, basi muabuduni, enyi watu, Peke Yake, Asiye na mshirika.
Ərəbcə təfsirlər:
وَتَقَطَّعُوٓاْ أَمۡرَهُم بَيۡنَهُمۡۖ كُلٌّ إِلَيۡنَا رَٰجِعُونَ
Lakini watu walitafautiana juu ya Mitume wao, na wengi wa wafauasi wao katika dini walipambanukana wakawa ni makundi na mapote, wakaabudu viumbe na matamanio. Na wote hao ni wenye kurejea kwetu na ni wenye kuhesabiwa juu ya yale waliyoyafanya.
Ərəbcə təfsirlər:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِنَ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَهُوَ مُؤۡمِنٞ فَلَا كُفۡرَانَ لِسَعۡيِهِۦ وَإِنَّا لَهُۥ كَٰتِبُونَ
Basi Mwenye kujilazimisha kumuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake na akafanya awezayo ya matendo mema kwa kumtii Mwenyezi Mungu na kumuabudu. Kwani Mwenyezi Mungu Hayapotezi matendo Yake wala Hayabatilishi, bali Anayaongeza yote hayo mara nyingi, na atayakuta aliyoyatenda kwenye Kitabu chake siku atakayofufuliwa baada ya kufa kwake.
Ərəbcə təfsirlər:
وَحَرَٰمٌ عَلَىٰ قَرۡيَةٍ أَهۡلَكۡنَٰهَآ أَنَّهُمۡ لَا يَرۡجِعُونَ
Haiwezekani kwa watu wa miji tuliyoiangamiza, kwa sababu ya ukanushaji wao na dhulma zao, kurudi duniani kabla ya Siku ya Kiyama ili kurakibisha kasoro zao ambazo walikuwa nazo.
Ərəbcə təfsirlər:
حَتَّىٰٓ إِذَا فُتِحَتۡ يَأۡجُوجُ وَمَأۡجُوجُ وَهُم مِّن كُلِّ حَدَبٖ يَنسِلُونَ
Basi pindi kitakapofunguliwa kizuizi cha Ya’jūj na Ma’jūj, na wakatoka kwenye ardhi za juu wakaenea kwenye pande zake kwa haraka,
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱقۡتَرَبَ ٱلۡوَعۡدُ ٱلۡحَقُّ فَإِذَا هِيَ شَٰخِصَةٌ أَبۡصَٰرُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يَٰوَيۡلَنَا قَدۡ كُنَّا فِي غَفۡلَةٖ مِّنۡ هَٰذَا بَلۡ كُنَّا ظَٰلِمِينَ
hapo Siku ya Kiyama itakuwa imekaribia na vituko vyake vitajitokeza, na hapo utayaona macho ya makafiri yamekodoka hayapepesi kwa kibabaiko kikali, huku wakiwa wanajiapiza maangamivu kwa majuto wakisema, «Ee ole wetu! Kwa hakika tulikuwa tumeghafilika na Siku hii na kujiandalia nayo na kwa hivyo tulikuwa madhalimu.»
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ حَصَبُ جَهَنَّمَ أَنتُمۡ لَهَا وَٰرِدُونَ
Kwa hakika, nyinyi, enyi makafiri, na vitu ambavyo mlikuwa mkiviabudu badala ya Mwenyezi Mungu, miongoni mwa masanamu, na wale walioridhia muwaabudu, kati ya majini na binadmu, ni viwashio vya moto wa Jahanamu na ni kuni zake, nyinyi na wao humo mtaingia.
Ərəbcə təfsirlər:
لَوۡ كَانَ هَٰٓؤُلَآءِ ءَالِهَةٗ مَّا وَرَدُوهَاۖ وَكُلّٞ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Lau hawa ambao mliwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka walikuwa ni waungu wanaostahiki kuabudiwa, hawangaliingia moto wa Jahanamu pamoja na nyinyi, enyi washirikina. Kwa hakika, wote hao, waabudu na waabudiwa, ni wenye kukaa milele ndani ya moto wa Jahanamu.
Ərəbcə təfsirlər:
لَهُمۡ فِيهَا زَفِيرٞ وَهُمۡ فِيهَا لَا يَسۡمَعُونَ
Hawa wenye kuadhibiwa Motoni wataona uchungu unaooneshwa na mlio wa sauti zao ambapo pumzi zao zinatoka kwa nguvu sana kutoka kwenye vifua vyao. Na wao wakiwa Motoni hawasikii kwa ukali wa adhabu wanayopewa.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ ٱلَّذِينَ سَبَقَتۡ لَهُم مِّنَّا ٱلۡحُسۡنَىٰٓ أُوْلَٰٓئِكَ عَنۡهَا مُبۡعَدُونَ
Kwa hakika, wale ambao kimetangulia kwetu sisi kitangulizi chema katika ujuzi wetu kuwa watakuwa ni watu wa Peponi, hao wataepushwa na Moto, hawataungia wala hawatakuwa karibu nao.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Ənbiya
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. - Tərcumənin mündəricatı

Tərcümə edən: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkir və Şeyx Nasir Xamis.

Bağlamaq