Check out the new design

Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Ənkəbut   Ayə:
وَمَا هَٰذِهِ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا لَهۡوٞ وَلَعِبٞۚ وَإِنَّ ٱلدَّارَ ٱلۡأٓخِرَةَ لَهِيَ ٱلۡحَيَوَانُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Na haukuwa uhai huu wa ulimwengu isipokuwa ni pumbao na mchezo wa kuzifanya nyoyo zipumbae na miili icheza, kwa sababu ya pambo na matamanio, kisha yanaondoka haraka. Na kwa hakika, nyumba ya Akhera ndiyo uhai wa kikweli na wa daima usikokuwa na kifo ndani yake. Lau watu wanalijua hilo hawangalifadhilisha nyumba ya kutoweka juu ya Nyumba ya kusalia.
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِذَا رَكِبُواْ فِي ٱلۡفُلۡكِ دَعَوُاْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ فَلَمَّا نَجَّىٰهُمۡ إِلَى ٱلۡبَرِّ إِذَا هُمۡ يُشۡرِكُونَ
Na wanapopanda makafiri kwenye majahazi baharini, na wakaogopa kuzama, wanampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtakasia dua wakati wa shida yao. Na Anapowaokoa akawafikisha kwenye nchi kavu, na shida ikawaondokea, wanarudi kwenye ushirikina wao. Hakika yao wao, kwa kufanya hivi, wanagongana, wanampwekesha Mwenyezi Mungu kipindi cha shida na wanamshirikisha kipindi cha raha.
Ərəbcə təfsirlər:
لِيَكۡفُرُواْ بِمَآ ءَاتَيۡنَٰهُمۡ وَلِيَتَمَتَّعُواْۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Na kushirikisha kwao baada ya sisi kuwaneemesha kwa kuwaokoa na bahari, ni ili iwe mwisho wake ni kuzikanusha zile tulizowaneemesha katika nafsi zao na mali zao na ili wakamilishe kujistarehesha kwao katika hii dunia. Basi wataujua uharibikaji wa matendo yao na kile Alichowaandalia wao Mwenyezi Mungu cha adhabu kali Siku ya Kiyama. Na katika hilo pana onyo na tahadharisho kwao.
Ərəbcə təfsirlər:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا جَعَلۡنَا حَرَمًا ءَامِنٗا وَيُتَخَطَّفُ ٱلنَّاسُ مِنۡ حَوۡلِهِمۡۚ أَفَبِٱلۡبَٰطِلِ يُؤۡمِنُونَ وَبِنِعۡمَةِ ٱللَّهِ يَكۡفُرُونَ
Kwani hawakushuhudia makafiri wa Makkah kwamba Mwenyezi Mungu Amewawekea Makkah kuwa ni mahali patakatifu penye amani, watu wake wanapata amani humo ya nafsi zao na mali zao, hali watu walio pambizoni mwake, nje ya eneo takatifu, wananyakuliwa hawana amani? Je, ni ushirikina wanaouamini na ni neema ya Mwenyezi Mungu Aliyowahusu wao nayo, wanayoikanusha, wakawa hawamuabudu Yeye, Peke Yake, bila mwingine?
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُۥٓۚ أَلَيۡسَ فِي جَهَنَّمَ مَثۡوٗى لِّلۡكَٰفِرِينَ
Hakuna yoyote aliye na udhalimu mkubwa kuliko yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu na akamnasibishia Mwenyezi Mungu upotevu alio nao na ubatilifu, au akaikanusha haki ambayo Mwenyezi Mungu Amemleta nayo Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Hakika ndani ya Moto ni makao ya aliyemkanusha Mwenyezi Mungu na akaukataa upweke Wake na akamkanusha Mtume Wake Muhammad,rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ فِينَا لَنَهۡدِيَنَّهُمۡ سُبُلَنَاۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَمَعَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na Waumini waliopigana jihadi na maadui wa Mwenyezi Mungu, nafsi na Shetani na wakavumilia kwenye misukosuko na makero katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Atawaongoa kwenye wema na kuwasimamisha imara juu ya njia iliyolingana sawa. Na yoyote ambaye sifa yake ni hii, basi yeye amejifanyia wema nafsi yake na amewafanyia wema wengine. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kuwa juu, Yupo pamoja na wale viumbe wake waliofanya wema, kwa kuwapa ushindi, kuwatilia nguvu, kuwahifadhi na kuwaongoza.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Ənkəbut
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. - Tərcumənin mündəricatı

Tərcümə edən: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkir və Şeyx Nasir Xamis.

Bağlamaq