Check out the new design

Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: Səba   Ayə:
لَقَدۡ كَانَ لِسَبَإٖ فِي مَسۡكَنِهِمۡ ءَايَةٞۖ جَنَّتَانِ عَن يَمِينٖ وَشِمَالٖۖ كُلُواْ مِن رِّزۡقِ رَبِّكُمۡ وَٱشۡكُرُواْ لَهُۥۚ بَلۡدَةٞ طَيِّبَةٞ وَرَبٌّ غَفُورٞ
Kwa hakika, kabila la Saba’ la huko Yaman, kwenye makazi ya watu wake kuna dalili ya uweza wetu: mabustani mawili kuliani na kushotoni, «Kuleni riziki ya Mola wenu na mumshukuruni kwa neema Zake juu yenu, kwani nchi yenu ina mchanga bora na hewa nzuri, na Mola wenu ni Mwingi wa msamaha kwenu.»
Ərəbcə təfsirlər:
فَأَعۡرَضُواْ فَأَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ سَيۡلَ ٱلۡعَرِمِ وَبَدَّلۡنَٰهُم بِجَنَّتَيۡهِمۡ جَنَّتَيۡنِ ذَوَاتَيۡ أُكُلٍ خَمۡطٖ وَأَثۡلٖ وَشَيۡءٖ مِّن سِدۡرٖ قَلِيلٖ
Wakaipa mgongo amri ya Mwenyezi Mungu, wakaacha kumshukuru na wakawakanusha Mitume, tukawatumia mafuriko yenye kubomoa yaliyo na nguvu, yaliyoliharibu bwawa la maji na yakayazamisha mabustani. Na tukawageuzia mabustani yao mawili yenye kutoa matunda yakawa ni mabustani mawili yenye miti michache ya khamṭ, nayo ni miti ya matunda machungu yenye ladha ya kuchukiza, na athl, nayo ni miti inayofanana na ṭarfā ’isiyokuwa na matunda, na mikunazi michache yenye miba mingi.
Ərəbcə təfsirlər:
ذَٰلِكَ جَزَيۡنَٰهُم بِمَا كَفَرُواْۖ وَهَلۡ نُجَٰزِيٓ إِلَّا ٱلۡكَفُورَ
Mabadiliko hayo, kutoka kwenye mambo mazuri kwenda kwenye mabaya, ni kwa sababu ya kukanusha kwao na kutoshukuru kwao neema za Mwenyezi Mungu. Na hatumtesi mateso haya makali isipokuwa mkanushaji sana aliyeendelea kwenye ukanushaji; atalipwa kulingana na matendo yake, sawa kwa sawa.
Ərəbcə təfsirlər:
وَجَعَلۡنَا بَيۡنَهُمۡ وَبَيۡنَ ٱلۡقُرَى ٱلَّتِي بَٰرَكۡنَا فِيهَا قُرٗى ظَٰهِرَةٗ وَقَدَّرۡنَا فِيهَا ٱلسَّيۡرَۖ سِيرُواْ فِيهَا لَيَالِيَ وَأَيَّامًا ءَامِنِينَ
Na tulijaalia, baina ya watu wa Saba’ na hali wao wako Yaman, na ile miji tuliobarikia, nayo ni Shām, kuwe na miji iliyoshikana, aliye kwenye mji wowote kati ya hiyo huuona mji mwingine. Na tukafanya mwendo wa kutembea humo ni mwendo uliokadiriwa, kutoka nyumba hadi nyumba, bila mashaka, na tukawaambia, «Endeni kwenye miji hiyo , wakati mnapotaka wa usiku au mchana, mkiwa mko kwenye amani hamuogopi adui, njaa wala kiu.
Ərəbcə təfsirlər:
فَقَالُواْ رَبَّنَا بَٰعِدۡ بَيۡنَ أَسۡفَارِنَا وَظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَجَعَلۡنَٰهُمۡ أَحَادِيثَ وَمَزَّقۡنَٰهُمۡ كُلَّ مُمَزَّقٍۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّكُلِّ صَبَّارٖ شَكُورٖ
Kwa sababu ya kuruka mipaka kwao, walichoka na raha na amani na maisha ya neema na wakasema, «Mola wetu! Ifanye miji yetu iwe mbali mbali ili safari zetu zirefuke baina ya miji hiyo, tusipate mji ulioimarika njiani tunapokwenda.» Na wakajidhulumu nafsi zao kwa kukanusha kwao, na kwa hivyo tukawaangamiza na tukawafanya ni mazingatio na mazungumzo kwa wanaokuja baada yao, na tukawatenganisha kila namna ya kuwatenganisha, na miji yao ikawa magofu. Kwa hakika yale yaliyoikumba Saba’ ni mazingatio kwa kila mwingi wa uvimilivu juu ya shida na mambo magumu, mwingi wa kushukuru neema za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
Ərəbcə təfsirlər:
وَلَقَدۡ صَدَّقَ عَلَيۡهِمۡ إِبۡلِيسُ ظَنَّهُۥ فَٱتَّبَعُوهُ إِلَّا فَرِيقٗا مِّنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na kwa hakika alidhani Iblisi dhana isiyo ya ukweli kuwa atawapoteza wanadamu na kwamba wao watamtii yeye katika kumuasi Mwenyezi Mungu, na dhana yake kwao ikawa ya kweli, kwa kuwa wao walimtii yeye na wakamuasi Mola wao , isipokuwa kundi la wenye kumuamini Mwenyezi Mungu, kwani wao walijikita kwenye utiifu wa Mwenyezi Mungu.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَا كَانَ لَهُۥ عَلَيۡهِم مِّن سُلۡطَٰنٍ إِلَّا لِنَعۡلَمَ مَن يُؤۡمِنُ بِٱلۡأٓخِرَةِ مِمَّنۡ هُوَ مِنۡهَا فِي شَكّٖۗ وَرَبُّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَفِيظٞ
Na wala hakuwa iblisi na uwezo wa kuwalazimisha wakanushaji kukufuru, lakini hekima ya Mwenyezi Mungu imepitisha awapambie wanadamu ili ujitokeze ujuzi Wake wa kale tupate kumpambanua anayeamini kufufuliwa, thawabu na adhabu na kumtenganisha na yule mwenye shaka na hilo. Na Mola wako ni Mtunzi wa kila jambo, Analihifadhi na kutoa malipo yake.
Ərəbcə təfsirlər:
قُلِ ٱدۡعُواْ ٱلَّذِينَ زَعَمۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَمۡلِكُونَ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا لَهُمۡ فِيهِمَا مِن شِرۡكٖ وَمَا لَهُۥ مِنۡهُم مِّن ظَهِيرٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie washirikina, «Waiteni wale ambao mlidai kuwa wao ni washirika wa Mwenyezi Mungu mkawaabudu badala Yake , miongoni mwa masanamu , malaika na binadamu, na wakusudieni katika haja zenu. Kwani wao hawatawaitika. Wao hawamiliki chochote, mbinguni wala ardhini, hata kadiri ya uzito wa chungu mdogo, na wala hawana ushirika katika hizo mbili. Na hakuna yoyote miongoni mwa hawa washirikina mwenye kumsaidia kuumba chochote. Bali Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, ndiye Aliyepwekeka kwa upatishaji.Yeye Ndiye Anayeabudiwa Peke Yake, na hakuna mwingine yoyote asiyekuwa Yeye anayestahiki kuabudiwa.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: Səba
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. - Tərcumənin mündəricatı

Tərcümə edən: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkir və Şeyx Nasir Xamis.

Bağlamaq