Check out the new design

Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Mursəlat   Ayə:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Je kwani sisi hatukuwaumba nyinyi, enyi mkusanyiko wa makafiri, kutokana na maji dhaifu yaliyo matwevu nayo ni tone la manii,
Ərəbcə təfsirlər:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
tukayaweka maji haya kwenye mahali palipohifadhika, napo ni kizazi cha mwanamke,
Ərəbcə təfsirlər:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
mpaka kipindi maalumu kinachojulikana na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka?
Ərəbcə təfsirlər:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukaweza kumuumba, kumtia sura na kumtoa. Basi bora wa wenye kuweza ni s isi.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kukanusha uweza wetu.
Ərəbcə təfsirlər:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Je kwani hatukuifanya hii ardhi mnayoishi juu yake
Ərəbcə təfsirlər:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
ikusanye juu ya mgongo wake walio hai wasiohesabika, na ndani ya matumbo yake wafu wasiodhibitika, na
Ərəbcə təfsirlər:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
tukajaalia iwe na majabali yaliyojikita yaliyo marefu ili isitikisike na nyinyi, na tukawanywesha maji tamu yaliyo mazuri?
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa waliozikanusha neema hizi.
Ərəbcə təfsirlər:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Wataambiwa makafiri Siku ya Kiyama, «Endeni kwenye adhabu ya moto wa Jahanamu mliokuwa mkiukanusha duniani.
Ərəbcə təfsirlər:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Endeni mjifinike kwenye kivuli cha moshi wa moto wa Jahanamu ambacho hapo panachembuka vipande vitatu.
Ərəbcə təfsirlər:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Kivuli hiko hakimfanyi mtu ahifadhike na joto la Siku hiyo wala hakizuii muwako wa Moto chochote.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika moto wa Jahanamu unarusha macheche makubwa ya moto, kila cheche moja katika hayo ni kama jengo lililoimarishwa katika ukubwa na urefu wa kuenda juu.
Ərəbcə təfsirlər:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba hizo cheche za moto wa Jahanamu zinazopaa juu ni ngamia weusi ambao rangi yao imeingia kwenye umanjano.»
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kukanusha mateso yaliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu.
Ərəbcə təfsirlər:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ndiyo Siku ya Kiyama ambayo wakanushaji hawatatamka maneno ya kuwanufaisha
Ərəbcə təfsirlər:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
wala hawatapewa idhini ya kusema wakatoa nyudhuru, kwa kuwa hawatakuwa na udhuru wowote.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kuikanusha siku hii na yaliyomo ndani yake.
Ərəbcə təfsirlər:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ni Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atatoa uamuzi baina ya viumbe, na ukweli na ubatilifu utapambanuka. Tutawakusanya nyinyi Siku hiyo, enyi makafiri wa ummah huu, pamoja na makafiri wa mwanzo miongoni mwa ummah waliopita.
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
Basi mkiwa na hila za kujitoa na adhabu, tumieni hila zenu na mziokoe nafsi zenu na msukosuko wa Mwenyezi Mungu na mateso Yake.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Kiyama.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika ya wale waliomuogopa Mola wao duniani na wakaiogopa adhabu Yake kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Wao Siku ya Kiyama watakuwa kwenye vivuli vya miti vilivyonyoka, na chemchemi za maji zinazotembea,
Ərəbcə təfsirlər:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
na matunda mengi yanayopendwa na nafsi zao ambayo wao wanastarehe nayo. Hapo waambiwe,
Ərəbcə təfsirlər:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
«Kuleni chakula chenye ladha na mnyweni kinywaji chenye kufurahisha kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza duniani.»
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Sisi, kwa mfano wa malipo hayo makubwa, tutawalipa watu wema katika matendo yao na utiifu wao kwetu.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Malipo na Hesabu, na kuzikanusha sterehe na mateso yaliyomo Siku hiyo.
Ərəbcə təfsirlər:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kisha Mwenyezi Mungu Akawaonya makafiri kwa kusema, «Kuleni aina ya vyakula vya ladha duniani na stareheni kwa matamanio yake yenye kumalizika kwa muda mchache, hakika nyinyi ni wahalifu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.»
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wanapoambiwa hawa washirikina, «Mswalieni Mwenyezi Mungu na mnyenyekeeni,» hawanyenyekei wala hawaswali, bali wanaendelea kuonyesha kiburi chao.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu.
Ərəbcə təfsirlər:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Iwapo wao hawataiamini hii Qur’ani, basi wataamini kitabu gani na maneno gani baada yake? Na Qur’ani yenyewe ni Kitabu kilichobainisha kila kitu, kilicho wazi katika hekima zake, hukumu zake na habari zake, chenye kushinda katika matamko yake na maana yake.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Mursəlat
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis. - Tərcumənin mündəricatı

Tərcümə edən: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkir və Şeyx Nasir Xamis.

Bağlamaq