Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Əli Muhsin Əl-Bervani * - Tərcumənin mündəricatı

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Mənaların tərcüməsi Surə: ən-Naziat   Ayə:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu!
Ninaapa kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuving'oa vitu kutokana na pahala pao kwa nguvu,
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa wanao toa kwa upole!
Na kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuvitoa vitu kwa utaratibu na ulaini,
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na wanao ogelea!
Na kwa kila kilicho pewa mbio za kutekeleza kazi yake kwa sahala na wepesi.
Ərəbcə təfsirlər:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Wakishindana mbio!
Na kwa vinavyo shindania kutimiza waajibu ulio twikwa juu yao kushindania kwa juhudi,
Ərəbcə təfsirlər:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Wakidabiri mambo.
Na vinavyo dabiri, kupanga, mambo na kuyaendesha kwa mujibu wa vilivyo khusishwa,
Ərəbcə təfsirlər:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka!
Bila ya shaka Saa ya Kiyama itafika; hiyo siku ambayo mpulizo wa mwanzo wa barugumu utavitikisa viumbe vyote,
Ərəbcə təfsirlər:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia.
Na mpulizo huo utafuatiwa na wa pili ambao ndio utakao kuwa wa kufufuliwa watu.
Ərəbcə təfsirlər:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga!
Siku hiyo nyoyo zitapapatika kwa khofu.
Ərəbcə təfsirlər:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho yatainama chini!
Macho ya watu yatakuwa na huzuni, manyonge.
Ərəbcə təfsirlər:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
Watu hawa husema duniani kwa kukanya kufufuliwa: Ati tutarudishwa sisi baada ya kwisha kufa, tuumbwe tena kama tulivyo kuwa?
Ərəbcə təfsirlər:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
Tukisha kuwa mafupa yaliyo chakaa, ati tutarejeshwa tufufuliwe upya?
Ərəbcə təfsirlər:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
Wanasema, kwa kukanya na kejeli: Kurejea huko kama kukitokea basi ni marejeo ya khasara, na sisi si watu wa kukhasiri.
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
Msidhani kurejea huko ni kuzito. Kwani hayo ni ukelele mmoja tu,
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
Mara maiti wote watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko!
Ərəbcə təfsirlər:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Ewe Muhammad! Imekufikilia hadithi ya Musa,
Ərəbcə təfsirlər:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
Alipo mwita Mola wake Mlezi katika bonde lilio takaswa, linalo itwa "T'uwa"?
Ərəbcə təfsirlər:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri
Akaambiwa: Nenda kwa Firauni aliye pindukia mpaka katika udhalimu.
Ərəbcə təfsirlər:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
Umwambie: Je! Huelekei kut'ahirika?
Ərəbcə təfsirlər:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
Na mimi nikuongoze upate kumjua Mola wako Mlezi, umwogope.
Ərəbcə təfsirlər:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
Musa akamwonyesha Firauni miujiza mikubwa.
Ərəbcə təfsirlər:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
Lakini Firauni alimkadhibisha Musa kwa aliyo kuja nayo, na akamuasi kwa aliyo mwitia.
Ərəbcə təfsirlər:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
Kisha akamgeuzia mgongo, akenda kujitahidi kumpinga.
Ərəbcə təfsirlər:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Akakusanya watu akanadi.
Akawakusanya wachawi, na akawaita watu,
Ərəbcə təfsirlər:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa.
Ərəbcə təfsirlər:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
Mwenyezi Mungu akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa a.s.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
Hakika katika hadithi hiyo yapo mawaidha kwa mwenye kumkhofu Mwenyezi Mungu.
Ərəbcə təfsirlər:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
Enyi mnao kanya kufufuliwa! Kukuumbeni nyinyi ni taabu zaidi au kuziumba mbingu, kuzikusanya sehemu zake zilio tawanyika mbali mbali,
Ərəbcə təfsirlər:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
Na kunyanyua kimo chake, na zikakaa sawa hazina tafauti wala ila?
Ərəbcə təfsirlər:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake
Na akatia kiza katika usiku wake, na akautokeza mchana wake ukawa na mwangaza?
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
Na ardhi baada ya hayo akaikunjua, na akaisawazisha, ikasilihi kukaliwa na watu wake?
Ərəbcə təfsirlər:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
Akatoa ndani yake maji yake yanayo tibuka katika chemchem zake, na ikamiminika mito yake, na ikawa na mimea yake ya chakula kwa ajili ya watu na wanyama;
Ərəbcə təfsirlər:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na milima akaisimamisha,
Na milima akaithibitisha imara
Ərəbcə təfsirlər:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
Kwa ajili ya manufaa yenu na wanyama wenu mnao wafuga!
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
Kitakapo fika Kiyama ambacho vitisho vyake vitaenea kote,
Ərəbcə təfsirlər:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
Siku atakapo kumbuka mtu vitendo vyake vya kheri au shari,
Ərəbcə təfsirlər:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
Na Jahannamu ikadhihirishwa wazi, akaiona kila mwenye macho kuwa ndio malipo,
Ərəbcə təfsirlər:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
Basi ama mwenye kupita mpaka kwa maasi yake,
Ərəbcə təfsirlər:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Na akakhiari maisha ya dunia,
Na akajichagulia nafsi yake maisha yanayo pita njia,
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
Basi Moto wa Jahannamu unao babua upepo wake ndio makaazi yake wala hana mengineyo.
Ərəbcə təfsirlər:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
Na ama mwenye kukhofu ukubwa na utukufu wa Mola wake Mlezi, na akaizuia nafsi yake na matamanio ya kumpumbaza,
Ərəbcə təfsirlər:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
Basi huyo nyumba ya neema ya Peponi ndio makaazi yake, wala hana penginepo.
Ərəbcə təfsirlər:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
Ewe Muhammad! Wanakuuliza, ati, khabari za Saa ya Kiyama, itakuwa lini?
Ərəbcə təfsirlər:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Una nini wewe hata uitaje?
Ujuzi wa hayo hauko kwako hata uwatajie.
Ərəbcə təfsirlər:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
Ujuzi wa hayo uko kwa Mola wako Mlezi tu, si kwa mwenginewe. (Nabii Isa a.s. ambaye Wakristo wanasema ni Mwana wa Mungu, au ndiye Mungu, pia anasimuliwa katika Biblia kuwa hakuijua Saa na Siku ya Kiyama. Injili ya Mathayo inanukulu maneno ya Yesu: "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.")
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
Kwani waajibu wako ni kuwaonya wanao khofu si kuwatangazia wakati wake.
Ərəbcə təfsirlər:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Na wao siku watakayo iona hiyo Saa ya Kiyama ni kama kwamba hawakuishi duniani zaidi kuliko jioni moja tu, au mchana wake.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: ən-Naziat
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Əli Muhsin Əl-Bervani - Tərcumənin mündəricatı

Qurani Kərimin səvahili dilinə mənaca tərcüməsi. Tərcümə etdi: Əli Muhsin Əl-Bərvani.

Bağlamaq