Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Vers: (152) Surah / Kapitel: Al -I-‘Imrân
وَلَقَدۡ صَدَقَكُمُ ٱللَّهُ وَعۡدَهُۥٓ إِذۡ تَحُسُّونَهُم بِإِذۡنِهِۦۖ حَتَّىٰٓ إِذَا فَشِلۡتُمۡ وَتَنَٰزَعۡتُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِ وَعَصَيۡتُم مِّنۢ بَعۡدِ مَآ أَرَىٰكُم مَّا تُحِبُّونَۚ مِنكُم مَّن يُرِيدُ ٱلدُّنۡيَا وَمِنكُم مَّن يُرِيدُ ٱلۡأٓخِرَةَۚ ثُمَّ صَرَفَكُمۡ عَنۡهُمۡ لِيَبۡتَلِيَكُمۡۖ وَلَقَدۡ عَفَا عَنكُمۡۗ وَٱللَّهُ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na kwa hakika Aliwahakikishia nyinyi Mwenyezi Mungu yale Aliyowaahidi ya kuwanusuru pindi mlipokuwa mnawaua makafiri katika vita vya uhud kwa idhini Yake Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Mpaka mlipokuwa waoga, mkawa madhaifu wa kupigana na mkatafautiana: je, mtasalia kwenye sehemu zenu za kivita au mtaziacha, ili mkusanye ngawira pamoja na wanaokusanya? Na mkaiasi amri ya Mtume wenu alipowaamrisha msiondoke kwenye sehemu zenu kwa vyovyote vile. Hapo ndipo pigo la kushindwa likawapata baada ya kuwaonesha mnayoyapenda ya ushindi, na ikadhihirika kuwa kati yenu kuna wanaotaka ngawira na kati yenu kuna wanaotaka Akhera na malipo yake. Kisha Mwenyezi Mungu Aliziepusha nyuso zenu na maadui wenu ili awape mtihani. Kwa hakika Aliyajua Mwenyezi Mungu majuto yenu na toba yenu, ndipo Akawasamehe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila kubwa kwa Waumini.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (152) Surah / Kapitel: Al -I-‘Imrân
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen