《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (152) 章: 阿里欧姆拉尼
وَلَقَدۡ صَدَقَكُمُ ٱللَّهُ وَعۡدَهُۥٓ إِذۡ تَحُسُّونَهُم بِإِذۡنِهِۦۖ حَتَّىٰٓ إِذَا فَشِلۡتُمۡ وَتَنَٰزَعۡتُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِ وَعَصَيۡتُم مِّنۢ بَعۡدِ مَآ أَرَىٰكُم مَّا تُحِبُّونَۚ مِنكُم مَّن يُرِيدُ ٱلدُّنۡيَا وَمِنكُم مَّن يُرِيدُ ٱلۡأٓخِرَةَۚ ثُمَّ صَرَفَكُمۡ عَنۡهُمۡ لِيَبۡتَلِيَكُمۡۖ وَلَقَدۡ عَفَا عَنكُمۡۗ وَٱللَّهُ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na kwa hakika Aliwahakikishia nyinyi Mwenyezi Mungu yale Aliyowaahidi ya kuwanusuru pindi mlipokuwa mnawaua makafiri katika vita vya uhud kwa idhini Yake Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Mpaka mlipokuwa waoga, mkawa madhaifu wa kupigana na mkatafautiana: je, mtasalia kwenye sehemu zenu za kivita au mtaziacha, ili mkusanye ngawira pamoja na wanaokusanya? Na mkaiasi amri ya Mtume wenu alipowaamrisha msiondoke kwenye sehemu zenu kwa vyovyote vile. Hapo ndipo pigo la kushindwa likawapata baada ya kuwaonesha mnayoyapenda ya ushindi, na ikadhihirika kuwa kati yenu kuna wanaotaka ngawira na kati yenu kuna wanaotaka Akhera na malipo yake. Kisha Mwenyezi Mungu Aliziepusha nyuso zenu na maadui wenu ili awape mtihani. Kwa hakika Aliyajua Mwenyezi Mungu majuto yenu na toba yenu, ndipo Akawasamehe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila kubwa kwa Waumini.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (152) 章: 阿里欧姆拉尼
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭