Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Vers: (10) Surah / Kapitel: Al-Fath
إِنَّ ٱلَّذِينَ يُبَايِعُونَكَ إِنَّمَا يُبَايِعُونَ ٱللَّهَ يَدُ ٱللَّهِ فَوۡقَ أَيۡدِيهِمۡۚ فَمَن نَّكَثَ فَإِنَّمَا يَنكُثُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦۖ وَمَنۡ أَوۡفَىٰ بِمَا عَٰهَدَ عَلَيۡهُ ٱللَّهَ فَسَيُؤۡتِيهِ أَجۡرًا عَظِيمٗا
Hakika ya hao wanaokupa mkono , ewe Mtume, wa ahadi ya kupigana hapo Ḥudaybiyah, wao kwa kweli wanampa mkono wa ahadi Mwenyezi Mungu na wanafanya mapatano na Yeye kwa kutaka Pepo Yake na radhi Zake. Mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao. Hivyo basi Yupo na wao anayasikia maneno yao, Anawaona mahali walipo na Anayajua mambo yao ya ndani na ya nje. Basi mwenye kuivunja ahadi yake aliyoitolea mkono, maangamivu ya jambo hilo yatamrudia mwenyewe; na atakayetekeleza ahadi aliyomuahidi Mwenyezi Mungu ya kuvumilia wakati wa mapambano na adui katika njia ya Mwenyezi Mungu na kumnusuru Nabii wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Mwenyezi Mungu Atampa malipo mema mengi, nayo ni Pepo. Katika aya pana kuthibitisha sifa ya mkono kwa Mwenyezi Mungu kwa namna inayonasibiana na Yeye, Aliyetakasika, bila kufananisha wala kueleza vile ulivyo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (10) Surah / Kapitel: Al-Fath
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen