Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Versículo: (10) Capítulo: Sura Al-Fath
إِنَّ ٱلَّذِينَ يُبَايِعُونَكَ إِنَّمَا يُبَايِعُونَ ٱللَّهَ يَدُ ٱللَّهِ فَوۡقَ أَيۡدِيهِمۡۚ فَمَن نَّكَثَ فَإِنَّمَا يَنكُثُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦۖ وَمَنۡ أَوۡفَىٰ بِمَا عَٰهَدَ عَلَيۡهُ ٱللَّهَ فَسَيُؤۡتِيهِ أَجۡرًا عَظِيمٗا
Hakika ya hao wanaokupa mkono , ewe Mtume, wa ahadi ya kupigana hapo Ḥudaybiyah, wao kwa kweli wanampa mkono wa ahadi Mwenyezi Mungu na wanafanya mapatano na Yeye kwa kutaka Pepo Yake na radhi Zake. Mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao. Hivyo basi Yupo na wao anayasikia maneno yao, Anawaona mahali walipo na Anayajua mambo yao ya ndani na ya nje. Basi mwenye kuivunja ahadi yake aliyoitolea mkono, maangamivu ya jambo hilo yatamrudia mwenyewe; na atakayetekeleza ahadi aliyomuahidi Mwenyezi Mungu ya kuvumilia wakati wa mapambano na adui katika njia ya Mwenyezi Mungu na kumnusuru Nabii wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Mwenyezi Mungu Atampa malipo mema mengi, nayo ni Pepo. Katika aya pana kuthibitisha sifa ya mkono kwa Mwenyezi Mungu kwa namna inayonasibiana na Yeye, Aliyetakasika, bila kufananisha wala kueleza vile ulivyo.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (10) Capítulo: Sura Al-Fath
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar