Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Übersetzungen

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Übersetzung der Bedeutungen Vers: (165) Surah / Kapitel: Al-An‘âm
وَهُوَ ٱلَّذِي جَعَلَكُمۡ خَلَٰٓئِفَ ٱلۡأَرۡضِ وَرَفَعَ بَعۡضَكُمۡ فَوۡقَ بَعۡضٖ دَرَجَٰتٖ لِّيَبۡلُوَكُمۡ فِي مَآ ءَاتَىٰكُمۡۗ إِنَّ رَبَّكَ سَرِيعُ ٱلۡعِقَابِ وَإِنَّهُۥ لَغَفُورٞ رَّحِيمُۢ
Naye ndiye aliye kufanyeni makhalifa wa duniani, na amewanyanyua baadhi yenu juu ya wengine daraja kubwa kubwa, ili akujaribuni kwa hayo aliyo kupeni. Hakika Mola Mlezi wako ni Mwepesi wa kuadhibu, na hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Na Yeye Mwenyezi Mungu ndiye aliye kufanyeni makhalifa (walio chukua pahala pa) kaumu zilizo tangulia katika kuamirisha ulimwengu. Naye amewanyanyua baadhi yenu kuliko wengine kwa daraja nyingi katika mambo yanayo onekana na yasiyo onekana kwa vile kukupeni njia za kuyafikilia, ili apate kukujaribuni, kukufanyieni mtihani, katika hizo neema alizo kupeni, vipi mtazishukuru, na katika sharia alizo kupeni mtazitumia vipi. Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwepesi wa kuwaadhibu wakhalifu, kwani hakika adhabu yake itakuja tu bila ya shaka, na kila lijalo lipo karibu. Na Yeye ni mwenye maghfira makubwa kwa makosa ya wenye kutubu na wakatengenea, na Mkunjufu wa rehema kwao.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (165) Surah / Kapitel: Al-An‘âm
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Schließen