Check out the new design

Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani. * - Übersetzungen

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: At-Tīn   Vers:

At-Tin

وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni! [1]
[1] Naapa kwa tini na zaituni, kwa baraka zao na ubora wa manufaa yao.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai! [2]
[2] Na kwa mlima ambao juu yake ndio Mwenyezi Mungu alimsemeza Musa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani! [3]
[3] Na kwa huu mji mtukufu wa Makka, ambao anaushuhudia utukufu wake mwenye kwenda uzuru, na anapata amani mwenye kuuingia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. [4]
[4] Kwa hakika bila ya shaka yoyote Sisi tumemuumba mtu amesimama sawa kwa umbo bora kabisa lilio nyooka, na akasifika kwa sifa nzuri kabisa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! [5]
[5] Kisha tukamteremsha cheo mpaka akawa ni wa chini kabisa katika hao walioko chini, kwa kuacha kufanya waajibu wa hayo tuliyo muumbia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. [6]
[6] Lakini walio amini na wakatenda vitendo vyema, hao basi watapata ujira usio wakatikia wala kuwapungukia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? [7]
[7] Basi kitu gani kinacho kupelekea kukadhibisha kufufuliwa na kulipwa baada ya kuwekwa wazi uweza wetu wa hayo?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? [8]
[8] Kwani Mwenyezi Mungu aliye yatenda hayo tuliyo kueleza si muadilifu kuliko mahakimu wote kwa kufanya na kupanga?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: At-Tīn
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani. - Übersetzungen

Übersetzung von Ali Muhsin Al-Barwani.

Schließen