Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (93) Surah: Yūnus
وَلَقَدۡ بَوَّأۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ مُبَوَّأَ صِدۡقٖ وَرَزَقۡنَٰهُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ فَمَا ٱخۡتَلَفُواْ حَتَّىٰ جَآءَهُمُ ٱلۡعِلۡمُۚ إِنَّ رَبَّكَ يَقۡضِي بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فِيمَا كَانُواْ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ
Hakika tuliwashukisha Wana wa Isrāīl mashukio mazuri yaliyoteuliwa katika miji ya Sham na Misri na tukawaruzuku riziki ya halali iliyo nzuri itokanayo na mazuri ya ardhi iliyobarikiwa. Na hawakutafautiana, katika mambo ya Dini yao isipokuwa baada ya kujiwa na ujuzi wa kuwafanya wao wawe pamoja na washikane, miongoni mwao ni yale yaliyomo ndani ya Taurati kuhusu habari ya unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye. Kwa kweli, Mola wako, ewe Mtume, Atahukumu baina yao Siku ya Kiyama na Atatoa uamuzi katika yale waliokuwa wakitafautiana juu yake kuhusu mambo yako, wapate kuingia wakanushaji Motoni na Waumini Peponi.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (93) Surah: Yūnus
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close