Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (10) Surah: Ibrāhīm
۞ قَالَتۡ رُسُلُهُمۡ أَفِي ٱللَّهِ شَكّٞ فَاطِرِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ يَدۡعُوكُمۡ لِيَغۡفِرَ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُؤَخِّرَكُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗىۚ قَالُوٓاْ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا تُرِيدُونَ أَن تَصُدُّونَا عَمَّا كَانَ يَعۡبُدُ ءَابَآؤُنَا فَأۡتُونَا بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ
Mitume wao wakasema kuwaambia, «Je, pana shaka yoyote juu ya Mwenyezi Mungu na kuwa Yeye Ndiye Muabudiwa Peke Yake, na hali Yeye ni Muumba wa mbingu na ardhi na Mwenye kuzifanya zipatikane kutoka kwenye hali ya kutokuwako bila ya kuwa na mfano uliotangulia, na hali Yeye Anawaita kwenye Imani Apate kuwasamehe mliyoyatanguliza ya ushirikina na Awaepushie adhabu ya kumaliza kabisa, Awape nafasi ya kusalia ulimwenguni mpaka muda Aliyoupanga ambao ni kikomo cha nyakati za maisha yenu, Asiwaadhibu duniani? Wakawaambia Mitume wao, «Hatuwaoni nyinyi isipokuwa ni binadamu, hali zenu ni kama zetu, hamna ubora wowote juu yetu wa kuwafanya muwe Mitume. Mnataka kutuzuia kuviabudu vitu ambavyo baba zetu walikuwa wakiviabudu miongoni mwa masanamu na mizimu. Basi tuletee hoja iliyo wazi yenye kuonyesha usahihi wa yale mnayoyasema.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (10) Surah: Ibrāhīm
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close