Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Baqarah   Ayah:
وَمَآ أَنفَقۡتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوۡ نَذَرۡتُم مِّن نَّذۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُهُۥۗ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٍ
Mali yoyote mnayoyatoa na mengineyo, machache au mengi, au sadaka mnayoitoa kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, au mkajilazimisha nafsi zenu chochote, cha mali au kinginecho, basi Mwenyezi Mungu Anayajua hayo; na Yeye Ndiye Mwenye kuchungulia nia zenu, na Atawalipa kwa hayo. Na yoyote mwenye kuzuia haki ya Mwenyezi Mungu ni dhalimu. Na madhalimu hawana wenye kuwanusuru ambao watawazuia wasipate adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِن تُبۡدُواْ ٱلصَّدَقَٰتِ فَنِعِمَّا هِيَۖ وَإِن تُخۡفُوهَا وَتُؤۡتُوهَا ٱلۡفُقَرَآءَ فَهُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّـَٔاتِكُمۡۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Mkizidhihirisha zile mnazozitoa sadaka kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ni sadaka nzuri mliyoitoa. Na mkizitoa kwa siri mkawapa mafukara, ni bora zaidi kwenu kwa kuwa hivyo ni mbali na ria. Na katika utoaji sadaka pamoja na ikhlasi kuna kusamehewa madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu Anayajua mambo ya ndani; hakuna kinachofichika Kwake katika mambo yenu na Atamlipa kila mtu kwa amali yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
۞ لَّيۡسَ عَلَيۡكَ هُدَىٰهُمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَهۡدِي مَن يَشَآءُۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلِأَنفُسِكُمۡۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ ٱللَّهِۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ
Si jukumu lako, ewe Mtume, kuwapa makafiri taufiki ya uongofu, lakini Mwenyezi Mungu Anavifungua vifua vya Anaowataka kwa Dini Yake na kuwaafikia kuifuata. Na mali yoyote mnayoyatoa, nafuu yake itawarudia nyinyi wenyewe kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na Waumini hawatoi isipokuwa kwa kutafuta radhi ya Mwenyezi Mungu. Na mali yoyote mnayoyatoa, kwa kumtakasia Mwenyezi Mungu, mtapewa kikamilifu thawabu zake na hamtapunguziwa chochote katika hizo. Katika hii aya pana kuthibitisha sifa ya Uso kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakata na kila sifa pungufu (wajh Allah) kwa namna inayonasibiana na Yeye.
Arabic explanations of the Qur’an:
لِلۡفُقَرَآءِ ٱلَّذِينَ أُحۡصِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا يَسۡتَطِيعُونَ ضَرۡبٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ يَحۡسَبُهُمُ ٱلۡجَاهِلُ أَغۡنِيَآءَ مِنَ ٱلتَّعَفُّفِ تَعۡرِفُهُم بِسِيمَٰهُمۡ لَا يَسۡـَٔلُونَ ٱلنَّاسَ إِلۡحَافٗاۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ
Wapeni sadaka zenu mafukara Waislamu ambao hawawezi kusafiri kutafuta riziki, kwa kuwa wameshughulika na jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, ambao huwadhania wao wasiowajua kuwa hawahitaji sadaka kwa kuwa wamejizuia na kuomba.Utawajua kwa alama zao na athari ya uhitaji walionao. Hawaombi kabisa. Na wakiomba, kwa kukosa budi, hawaombi kwa utiriri. Na mali yoyote mnayoyatoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, hakuna chochote, katika hayo, chenye kufichika kwa Mwenyezi Mungu.Na Mwenyezi Mungu Atalipa kwayo malipo mengi zaidi na makamilifu zaidi Siku ya Kiyama.
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُم بِٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ فَلَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Wale ambao wanatoa mali zao kwa kumridhisha Mwenyezi Mungu, mchana na usiku, kwa siri na kwa dhahiri, watapata malipo yao mbele ya Mola wao, na wala hapana khofu juu yao kuhusu mambo watakayoyakabili Akhera wala hawatakuwa na huzuni juu ya vitu vya kidunia vilivyowapita wasivipate. Sheria hiyo ya Ki- Mungu yenye hekima, ndiyo njia ya Uislamu katika utoaji, yenye kuondoa mahitaji ya mafukara kwa heshima na utu, kusafisha mali ya matajiri na kuhakikisha kusaidiana juu ya wema na ucha-Mungu ili kutaka radhi za Mwenyezi Mungu bila maonevu au kulazimisha.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Baqarah
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close