Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (165) Surah: Āl-‘Imrān
أَوَلَمَّآ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَدۡ أَصَبۡتُم مِّثۡلَيۡهَا قُلۡتُمۡ أَنَّىٰ هَٰذَاۖ قُلۡ هُوَ مِنۡ عِندِ أَنفُسِكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Kwa nini mlipopatwa na msiba uliowakumba siku ya Uhud, ingawa mumewapata washirikina mara mbili yake siku ya Badr, mlisema kwa kustaajabu, «Mambo haya yatakuwa vipi, na sisi ni Waislamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu yuko na sisi, na hawa ni washirikina?» Sema uwaambie, ewe Nabii, «Haya yaliyowapata yamesababishwa na nyinyi wenyewe kwa kuenda kinyume kwenu na amri ya Mtume wenu na kuelekea kwenu kukusanya ngawira.» Kwa hakika, Mwenyezi Mungu Anafanya Atakalo na Anahukumu Atakavyo. Hakuna mwenye kuitangua hukumu Yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (165) Surah: Āl-‘Imrān
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close