Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (195) Surah: Āl-‘Imrān
فَٱسۡتَجَابَ لَهُمۡ رَبُّهُمۡ أَنِّي لَآ أُضِيعُ عَمَلَ عَٰمِلٖ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰۖ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۖ فَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَأُخۡرِجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَأُوذُواْ فِي سَبِيلِي وَقَٰتَلُواْ وَقُتِلُواْ لَأُكَفِّرَنَّ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَأُدۡخِلَنَّهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ ثَوَابٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥ حُسۡنُ ٱلثَّوَابِ
Na Mwenyezi Mungu Akaitikia maombi yao kwamba Yeye Hazipotezi juhudi za yoyote aliyetenda amali njema, awe ni mwanamume au ni mwanamke. Kwani wao, katika undugu wa kidini, kukubaliwa amali zao na kulipwa kwazo, ni sawa. Kwa hivyo, wale waliohama kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, wakatolewa kwenye majumba yao, wakaudhiwa katika kumtii Mola wao na kumuabudu kwao Yeye Peke Yake, wakapigana na wakauawa katikia njia ya Mwenyezi Mungu kwa kulikuza neno Lake, hao Mwenyezi Mungu Atawapa sitara kwa maasia waliyoyafanya kama Alivyowasitiri nayo duniani na Hatawahesabu kwayo. Na atawaingiza, tena Atawaingiza, kwenye mabustani ya Peponi ambayo inapita mito chini ya majumba yake ya fahari na miti yake. Hayo yakiwa ni malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo mazuri.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (195) Surah: Āl-‘Imrān
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close