Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (83) Surah: Āl-‘Imrān
أَفَغَيۡرَ دِينِ ٱللَّهِ يَبۡغُونَ وَلَهُۥٓ أَسۡلَمَ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ طَوۡعٗا وَكَرۡهٗا وَإِلَيۡهِ يُرۡجَعُونَ
Je, wanataka hawa wenye kutoka nje ya twaa ya Mwenyezi Mungu, miongoni mwa Watu wa Kitabu, dini isiyokuwa dini ya Mwenyezi Mungu nayo ni Uislamu ambao Mwenyezi Mungu Alimtumiliza nao Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hali ya kuwa wote walioko mbinguni na ardhini wamejisalimisha na kufuata na kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu kwa hiyari, kama walivyo Waumini, na kwa kulazimika wakati wa shida ambapo hilo haliwanufaishi, nao ni makafiri, kama vilivyonyenyekea Kwake viumbe vyote. Na Kwake watarejeshwa Siku ya Marejeo, na alipwe kila mmoja kwa amali yake? Hili ni onyo kutoka kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kwa yoyote, katika viumbe Vyake, atakayerudi Kwake juu ya mila isiyokuwa ya Kiislamu.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (83) Surah: Āl-‘Imrān
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close