Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (22) Surah: Saba’
قُلِ ٱدۡعُواْ ٱلَّذِينَ زَعَمۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَمۡلِكُونَ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا لَهُمۡ فِيهِمَا مِن شِرۡكٖ وَمَا لَهُۥ مِنۡهُم مِّن ظَهِيرٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie washirikina, «Waiteni wale ambao mlidai kuwa wao ni washirika wa Mwenyezi Mungu mkawaabudu badala Yake , miongoni mwa masanamu , malaika na binadamu, na wakusudieni katika haja zenu. Kwani wao hawatawaitika. Wao hawamiliki chochote, mbinguni wala ardhini, hata kadiri ya uzito wa chungu mdogo, na wala hawana ushirika katika hizo mbili. Na hakuna yoyote miongoni mwa hawa washirikina mwenye kumsaidia kuumba chochote. Bali Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, ndiye Aliyepwekeka kwa upatishaji.Yeye Ndiye Anayeabudiwa Peke Yake, na hakuna mwingine yoyote asiyekuwa Yeye anayestahiki kuabudiwa.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (22) Surah: Saba’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close