Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (18) Surah: An-Nisā’
وَلَيۡسَتِ ٱلتَّوۡبَةُ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ حَتَّىٰٓ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ إِنِّي تُبۡتُ ٱلۡـَٰٔنَ وَلَا ٱلَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمۡ كُفَّارٌۚ أُوْلَٰٓئِكَ أَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا
Kukubaliwa toba si kwa wale wanaoendelea kufanya maasia bila ya kurudi kwa Mola wao mpaka wakafikiwa na shida ya mauti, hapo mmoja wao aseme, «Mimi sasa nimetubia.» Kama ambavyo haikubaliwi toba ya wale wanaokufa na hali wao ni wenye kukanusha, ni wenye kupinga upweke wa Mwenyezi Mungu na ujumbe wa Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Hao wenye kuendeleza maasia hadi kufa kwao, na wakanushaji ambao wanakufa na huku ni makafiri, tumewatayarishia adhabu iumizayo.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (18) Surah: An-Nisā’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close