Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Ahqāf   Ayah:
وَإِذۡ صَرَفۡنَآ إِلَيۡكَ نَفَرٗا مِّنَ ٱلۡجِنِّ يَسۡتَمِعُونَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوٓاْ أَنصِتُواْۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوۡاْ إِلَىٰ قَوۡمِهِم مُّنذِرِينَ
Na kumbuka, ewe Mtume, pindi tulipokutumia kundi la majini kusikiliza Qur’ani kutoka kwako. Walipohudhuria, na Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, yuwasoma, waliambiana wao kwa wao, «Nyamazeni tusikilize Qur’ani! Na Mtume Alipomaliza kusoma Qur’ani, na wao wakawa wameielewa na ikawa imewaathiri, walirudi kwa majini wenzao wakawaonya na kuwahadharisha adhabu ya Mwenyezi Mungu wasipoamini.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالُواْ يَٰقَوۡمَنَآ إِنَّا سَمِعۡنَا كِتَٰبًا أُنزِلَ مِنۢ بَعۡدِ مُوسَىٰ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ وَإِلَىٰ طَرِيقٖ مُّسۡتَقِيمٖ
walisema, «Enyi jamaa zetu! Sisi tumesikia Kitabu kilichoteremshwa baada ya Mūsā, chenye kusadikisha Vitabu vya Mwenyezi Mungu vlivyokuwa kabla yake, ambavyo Mwenyezi Mungu Ameviteremsha kwa Mitume Wake, (Kitabu) ambacho kinaongoza kwenye haki na usawa na kwenye njia sahihi iliyonyoka.
Arabic explanations of the Qur’an:
يَٰقَوۡمَنَآ أَجِيبُواْ دَاعِيَ ٱللَّهِ وَءَامِنُواْ بِهِۦ يَغۡفِرۡ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُجِرۡكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٖ
«Enyi jamaa zetu! Muitikieni Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad kwa kile anachowaitia, na muaminini yeye na myafuate kivitendo yale aliyoyaleta, Mwenyezi Mungu Atawasamehe dhambi zenu na Atawaokoa na adhabu yenye uchungu inayoumiza.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَن لَّا يُجِبۡ دَاعِيَ ٱللَّهِ فَلَيۡسَ بِمُعۡجِزٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَيۡسَ لَهُۥ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءُۚ أُوْلَٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
«Na asiyemuitikia Mtume wa Mwenyezi Mungu katika yale aliyoyalingania, basi yeye hatamshinda Mwenyezi Mungu katika ardhi Akitaka kumuadhibu, wala hatakuwa na wasaidizi badala ya Mwenyezi Mungu, wenye kumkinga na adhabu Yake. Hao watakuwa wametoka nje ya haki waziwazi.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّ ٱللَّهَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَلَمۡ يَعۡيَ بِخَلۡقِهِنَّ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰۚ بَلَىٰٓۚ إِنَّهُۥ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Je, wameghafilika na wasijue kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyeumba mbingu na ardhi pasi na mfano uliotangulia na bila kuelemewa na kuziumba, ni Muweza wa kuhuisha wafu ambao Aliwaumba hapo mwanzo? Ndio, hilo ni jambo jepesi kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Ambaye hakuna chochote kinachomshinda. Hakika Yeye kwa kila jambo ni Muweza.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَيَوۡمَ يُعۡرَضُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ عَلَى ٱلنَّارِ أَلَيۡسَ هَٰذَا بِٱلۡحَقِّۖ قَالُواْ بَلَىٰ وَرَبِّنَاۚ قَالَ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ
Na Siku ya Kiyama, wataorodheshwa waliokufuru juu ya Moto wa Jahanamu ili waadhibiwe na waambiwe, «Je, hii adhabu si kweli?». watajibu kwa kusema, «Ndio. Tunaapa kwa Mola wetu kuwa hii ndiyo kweli.» Hapo waambiwe, «Basi onjeni adhabu kwa kuwa mlikuwa mkiikataa adhabu ya Moto na kuikanusha duniani.»
Arabic explanations of the Qur’an:
فَٱصۡبِرۡ كَمَا صَبَرَ أُوْلُواْ ٱلۡعَزۡمِ مِنَ ٱلرُّسُلِ وَلَا تَسۡتَعۡجِل لَّهُمۡۚ كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَ مَا يُوعَدُونَ لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا سَاعَةٗ مِّن نَّهَارِۭۚ بَلَٰغٞۚ فَهَلۡ يُهۡلَكُ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ
Basi vumilia, ewe Mtume, kwa yanayokupata ya makero ya watu wako wenye kukukanusha kama vile walivyovumilia Mitume wenye nia thabiti kabla yako wewe, nao, kwa kauli mashuhuri, ni Nūḥ, Ibrāhīm, Mūsā na Īsā, na wewe ni miongoni mwao, wala usiwafanyie haraka watu wako ya kuadhibiwa. Kwani itapotokea na wakaiona, watajihisi kama kwamba hawakukaa duniani isipokuwa muda mchache wa mchana. Haya ni mafikisho kwao na kwa wasiokuwa wao. Na haangamizwi kwa adhabu ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu waliotoka nie ya amri Yake na twaa Yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Ahqāf
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close