Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (20) Surah: Al-Hadīd
ٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا لَعِبٞ وَلَهۡوٞ وَزِينَةٞ وَتَفَاخُرُۢ بَيۡنَكُمۡ وَتَكَاثُرٞ فِي ٱلۡأَمۡوَٰلِ وَٱلۡأَوۡلَٰدِۖ كَمَثَلِ غَيۡثٍ أَعۡجَبَ ٱلۡكُفَّارَ نَبَاتُهُۥ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَىٰهُ مُصۡفَرّٗا ثُمَّ يَكُونُ حُطَٰمٗاۖ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ عَذَابٞ شَدِيدٞ وَمَغۡفِرَةٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرِضۡوَٰنٞۚ وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا مَتَٰعُ ٱلۡغُرُورِ
Jueni, enyi watu, kwamba uhai wa kilimwengu ni mchezo na pumbao ya miili kuchezea na nyoyo kupumbaa, na pambo la nyinyi kujipamba nalo, na kuoneshana baina yenu kwa vitu vyake vya starehe, na kushindana kwa wingi wa mali na watoto. Mfano wake ni kama ule wa mvua ambayo mimea yake iliwafurahisha wakulima, kisha ikasinyaa na kukauka, ukaiona imekuwa rangi ya manjano baada ya kuwa rangi ya kijani, kisha ikawa ni yenye kukatikakatika na kuwa mikavu na kusagikasagika. Na huko Akhera kuna adhabu kali kwa makafiri na msamaha wa Mwenyezi Mungu na radhi Zake kwa watu wenye kuamini. Na haukuwa uhai wa kilimwengu, kwa mwenye kuushughulikia hali ya kusahau Akhera yake, isipokuwa ni starehe yenye udanganyifu.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (20) Surah: Al-Hadīd
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close