Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (6) Surah: Yūsuf
وَكَذَٰلِكَ يَجۡتَبِيكَ رَبُّكَ وَيُعَلِّمُكَ مِن تَأۡوِيلِ ٱلۡأَحَادِيثِ وَيُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكَ وَعَلَىٰٓ ءَالِ يَعۡقُوبَ كَمَآ أَتَمَّهَا عَلَىٰٓ أَبَوَيۡكَ مِن قَبۡلُ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبَّكَ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
Na kadhaalika Mola wako Mlezi atakuteuwa na atakufundisha tafsiri ya mambo. Na atatimiza neema zake juu yako na juu ya ukoo wa Yaa'qub, kama alivyo watimizia hapo zamani baba zako Ibrahim na Is-haq. Hakika Mola wako Mlezi ni Mjuzi Mwenye hikima.
Kama ulivyo jiona katika ndoto kuwa ni bwana wa kut'iiwa, mwenye cheo na madaraka, basi Mola wako Mlezi atakuteuwa na atakukhitari, akufunze kufasiri ndoto, kwa kukupa Unabii na Utume, kama hapo zamani, kabla ya baba yako, Yaa'qub, alivyo wafanyia baba zako, Ibrahim na Is-haq. Hakika Mola wako Mlezi ni mwingi wa hikima, basi hakosei. Ni mwingi wa ujuzi, basi humteuwa katika waja wake anaye mjua kuwa anastahili kuteuliwa.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (6) Surah: Yūsuf
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close