Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (47) Surah: An-Nahl
أَوۡ يَأۡخُذَهُمۡ عَلَىٰ تَخَوُّفٖ فَإِنَّ رَبَّكُمۡ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٌ
Au hatawashika kwa kitisho na kuwapunguza kidogo kidogo? Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenye huruma, Mwenye kurehemu.
Au akawateremshia adhabu katika nafsi zao na mali yao kidogo kidogo, na hali wao kila wakati wa hiyo adhabu wamo katika khofu na kuingoja iwateremkie. Basi, enyi washirikina! Msiendelee, mkajidanganya kwa kuchelewa adhabu yenu! Upole wake Mwenyezi Mungu ulio enea, na rehema yake iliyo kunjuka, ndio iliyo hukumu asikuleteeni kwa haraka adhabu ya hapa duniani, ili mpate kufikiri na kuzingatia. Kwani Yeye Subhanahu ni Mpole na Mwenye kurehemu.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (47) Surah: An-Nahl
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close