Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (37) Surah: Al-Anbiyā’
خُلِقَ ٱلۡإِنسَٰنُ مِنۡ عَجَلٖۚ سَأُوْرِيكُمۡ ءَايَٰتِي فَلَا تَسۡتَعۡجِلُونِ
Mwanaadamu ameumbwa na haraka. Nitakuonyesheni Ishara zangu. Basi msinihimize.
Na ikiwa wao wanataka waletewe adhabu kwa upesi, basi ndio tabia ya binaadamu kutaka kila jambo kwa haraka. Basi enyi wenye haraka! Nitakuonesheni neema yangu duniani, na adhabu yangu Akhera. Msijishughulishe kuhimiza kitu ambacho hakina budi kuwa. Maoni ya wataalamu juu ya Aya 37: "Mwanaadamu ameumbwa na haraka. Nitakuonyesheni Ishara zangu. Basi msinihimize." Makusudio ya kauli ya "Ishara" ni ishara za maumbile zenye kuonyesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na uweza wake. Na ujuzi wa ilimu za sayansi utavumbua kwa mujibu wa itavyo nyanyuka akili ya binaadamu. Na hayo ni kwa mujibu wa miadi ilio wekwa kwa wakati wake. Kila ukifika wakati maalumu Mwenyezi Mungu hudhihirisha Ishara yake, au huwasahilishia wanaadamu njia za kuzifikilia Ishara hizo.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (37) Surah: Al-Anbiyā’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close