Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (26) Surah: Āl-‘Imrān
قُلِ ٱللَّهُمَّ مَٰلِكَ ٱلۡمُلۡكِ تُؤۡتِي ٱلۡمُلۡكَ مَن تَشَآءُ وَتَنزِعُ ٱلۡمُلۡكَ مِمَّن تَشَآءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَآءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَآءُۖ بِيَدِكَ ٱلۡخَيۡرُۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Sema: Ewe Mwenyezi Mungu uliye miliki ufalme wote! Wewe humpa ufalme umtakaye, na humwondolea ufalme umtakaye, na humtukuza umtakaye, na humuangusha umtakaye. Kheri yote iko mikononi mwako. Hakika Wewe ni Muweza wa kila kitu.
Ewe Nabii! Sema kwa unyenyekevu na kuukiri utukufu wake Mwenyezi Mungu: Ewe Mola Mlezi! Ni Wewe peke yako ndiye Mwenye kumiliki kutasarafu katika mambo yote. Unampa kuhukumu na utawala umtakaye, na unamnyima umtakaye. Unampa utukufu umpendaye kati ya waja wako kwa kumwezesha kuzishika sababu za kuufikia huo utukufu. Na unampiga madhila na unyonge umtakaye. Basi Wewe peke yako unamiliki kheri yote. Hushindwi na kitu katika kutimiza muradi wako na yanayo kupelekea hikima yako kuyakatia shauri katika mipango ya uumbaji wako.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (26) Surah: Āl-‘Imrān
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close