Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (44) Surah: Al-Anfāl
وَإِذۡ يُرِيكُمُوهُمۡ إِذِ ٱلۡتَقَيۡتُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِكُمۡ قَلِيلٗا وَيُقَلِّلُكُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِهِمۡ لِيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗاۗ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ
Na mlipo kutana akakuonyesheni machoni mwenu kuwa wao ni wachache, na akakufanyeni nyinyi ni wachache machoni mwao, ili Mwenyezi Mungu atimize jambo lilio kuwa liwe. Na mambo yote hurejezwa kwa Mwenyezi Mungu.
Na kumbuka, ewe Mtume! Alipo kuonyeshemi Mwenyezi Mungu kuwa maadui zenu mnapo kutatana nao ni wachache katika macho yenu, kama alivyo waonyesha wao kuwa nyinyi ni wachache, na kwa kuwa tangu hapo wao wana ghururi ndani ya nafsi zao kuwa ni wengi, ili kila mmoja wenu awanie kupigana na mwenzie, na kwa hivyo yatimie aliyo kwisha yaamrisha Mwenyezi Mungu. Na ilikuwa hapana budi hayo yatimie. Na kwa Mwenyezi Mungu ndio hurejea mambo yote ya ulimwengu. Halitendeki jambo ila alilo kwisha lihukumia na kuzitengeneza sababu zake.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (44) Surah: Al-Anfāl
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close