Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (57) Surah: Al-Anfāl
فَإِمَّا تَثۡقَفَنَّهُمۡ فِي ٱلۡحَرۡبِ فَشَرِّدۡ بِهِم مَّنۡ خَلۡفَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ
Basi ukiwakuta vitani wakimbize walio nyuma yao ili wapate kukumbuka.
Basi ewe Mtume! Ukiwakuta hawa wavunjao mapatano, na ukasadifiana nao katika vita nawe umeshinda, basi watishe baraabara kwa kuwapa adhabu ya kuwatia uchungu na kuwaogopesha wale walio nyuma yao, upate kuwafarikisha walio baki. Mateso haya ndiyo ya kuwakumbusha uovu wa kuvunja mapatano, na kuwazuia wenginewe wasitende kama hayo. Katika Aya tukufu hizi tunahadharishwa na wale wanao toa ahadi na kisha wakazivunja. Hawa yafaa wapewe adhabu ya kutia mfano kwao na kwa walio nyuma yao. Na katika Aya hii unabainishwa umuhimu wa kuvuruga askari wa adui walio nyuma. Hizi ni mbinu za vita za kisasa, kwani kuzua vurugo katika askari wa nyuma hutosha kuleta fujo na kupelekea jeshi kutawanya askari wake kulinda mgongo wake, na kwa hivyo zinavunjika nguvu zake. Juu ya hivyo katika sehemu za nyuma katika midani ndio huwapo mambo yaliyo khusu idara ya jeshi ambayo juu yake ndio jeshi linategemea kwa msaada. Ukileta vurugu hapa hupelekea kukosekana nidhamu yote ya jeshi, na kwa hivyo ndio huleta kuemewa na kushindwa.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (57) Surah: Al-Anfāl
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close