Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Versículo: (56) Capítulo: Sura Al-Israa
قُلِ ٱدۡعُواْ ٱلَّذِينَ زَعَمۡتُم مِّن دُونِهِۦ فَلَا يَمۡلِكُونَ كَشۡفَ ٱلضُّرِّ عَنكُمۡ وَلَا تَحۡوِيلًا
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina wa Makkah, «Hawa masanamu mnaowaita wawaondolee shida hawawezi hilo wala hawawezi kuiyepusha kwenu nyinyi kuipeleka kwa wengine, na pia hawawezi kuigeuza kutoka namna ilivyo kuifanya namna nyingine, Mwenye kuweza hilo ni Mwenyezi Mungu Peke Yake.» Aya hii inakusanya kila anayeombwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, miongoni mwa Manabii, watu wema na wasiokuwa hao, kwa tamko la istighāthah (kutaka uokozi) au du'a’ (maombi) au mfano wake, kwani hapana mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (56) Capítulo: Sura Al-Israa
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar