Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Versículo: (150) Capítulo: Sura Al-An'aam
قُلۡ هَلُمَّ شُهَدَآءَكُمُ ٱلَّذِينَ يَشۡهَدُونَ أَنَّ ٱللَّهَ حَرَّمَ هَٰذَاۖ فَإِن شَهِدُواْ فَلَا تَشۡهَدۡ مَعَهُمۡۚ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ وَهُم بِرَبِّهِمۡ يَعۡدِلُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Waleteni mashahidi wenu ambao watatoa ushahidi kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyeharamisha vile mlivyoviharamisha vya makulima na wanyama howa.» Wakitoa ushahidi huo, kwa urongo na uzushi, usiwaamini wala usikubaliane na wale waliojitolea uamuzi wenyewe kulingana na mapendeleo ya nafsi zao, wakazikanusha aya za Mwenyezi Mungu katika yale waliyoyashikilia ya kukiharamisha Alichokihalalisha Mwenyezi Mungu na kukihalalisha Alichokiharamisha Mwenyezi Mungu. Wala usiwafuate wale ambao hawayaamini maisha ya Akhera wala wasiotenda vitendo vya kuwafaa huko na wale ambao Mola wao wanamshirikisha wakawa wanamuabudu mwingine pamoja na Yeye.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (150) Capítulo: Sura Al-An'aam
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar