Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Versículo: (158) Capítulo: Sura Al-An'aam
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ أَوۡ يَأۡتِيَ رَبُّكَ أَوۡ يَأۡتِيَ بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَۗ يَوۡمَ يَأۡتِي بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَ لَا يَنفَعُ نَفۡسًا إِيمَٰنُهَا لَمۡ تَكُنۡ ءَامَنَتۡ مِن قَبۡلُ أَوۡ كَسَبَتۡ فِيٓ إِيمَٰنِهَا خَيۡرٗاۗ قُلِ ٱنتَظِرُوٓاْ إِنَّا مُنتَظِرُونَ
Kwani wanangojea, hawa wenye kukataa na wakazuia watu wasiifuate njia ya Mwenyezi Mungu, isipokuwa awajie wao Malaika wa mauti na wasaidizi wake kuzichukua roho zao au aje Mola wako, ewe Mtume, kutoa uamuzi kati ya waja wake Siku ya Kiyama, au zije baadhi ya alama za Kiyama na vitambulisho vyake vinavyoashiria kuja kwake, navyo ni kuchomoza jua kutoka upande wake wa Magharibi? Basi litakapokuwa hilo hakuna nafsi yoyote itakayofaidika na Imani yake, iwapo haikuwa imeamini kabla ya hapo, wala hayatakubaliwa matendo mema mapya ya hiyo nafsi, ikiwa ilikuwa imeamini, iwapo haikuwa imeyatenda kabla ya hapo. Waambie, ewe Mtume, «Ngojeeni kuja kwake, ili mpate kumjua aliye kwenye usawa na aliye kwenye makosa, na mtenda maovu na mtenda mema. Sisi tunalingojea hilo.»
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (158) Capítulo: Sura Al-An'aam
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar