Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Versículo: (54) Capítulo: Sura Al-An'aam
وَإِذَا جَآءَكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِنَا فَقُلۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۖ كَتَبَ رَبُّكُمۡ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَ أَنَّهُۥ مَنۡ عَمِلَ مِنكُمۡ سُوٓءَۢا بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ تَابَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَأَنَّهُۥ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na wakikujia, ewe Nabii, wale wanaoamini aya za Mwenyezi Mungu zenye kushuhudia ukweli wako juu ya Qur’ani na mengineyo, kutaka fatuwa kuhusu toba ya madhambi yao yaliyotangulia, basi wakirimu kwa kuwarudishia salamu na uwape bishara ya rehema ya Mwenyezi Mungu iliyo kunjufu. Kwani Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, Ametoa ahadi Yake Mwenyewe kuwarehemu waja Wake kwa kuwafanyia wema kwamba mwenye kufanya dhambi kwa kutojua mwisho wake mbaya na kuwa linapelekea kukasirikiwa na Mwenyezi Mungu-Basi kila mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu kwa kukosea au kwa kusudi huwa ni mjinga kwa mtizamo huu, ingawa ajua kuwa ni haramu- kisha baada yake akatubia na akaendelea kufanya matendo mema, basi Mwenyezi Mungu Atamsamehe dhambi lake, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe kwa waja Wake wenye kutubia, ni Mwingi wa rehema kwao.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (54) Capítulo: Sura Al-An'aam
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar