Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (6) Capítulo: Sura Yunus
إِنَّ فِي ٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ وَمَا خَلَقَ ٱللَّهُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَتَّقُونَ
Hakika katika kukhitalifiana usiku na mchana, na katika alivyo umba Mwenyezi Mungu katika mbingu na ardhi, zipo Ishara kwa watu wanao mcha-Mngu.
Hakika katika kufuatana usiku na mchana na kukhitalifiana kwao, kwa kuzidi na kupungua, na katika uumbaji wa mbingu na ardhi na vitu vyote viliomo humo, zipo dalili zilizo wazi na hoja zilizo dhaahiri zenye kuhakikisha Ungu wa Mwenye kuumba, na uwezo wake. Hayo ni kwa wenye kutaka kuiepuka ghadhabu yake na wakaiogopa adhabu yake. Aya hii ya 6 inaashiria hakika inayo onekana, nayo kukhitalifiana urefu wa usiku na mchana kwa mwaka mzima katika pahala popote duniani. Na kadhaalika kufuatana mchana na usiku, na kuwa mchana ni wa kuangaza na kuonana, na usiku ni giza. Na maana ya hayo ni kuwa msingi wake ni kuwa dunia inazunguka wenyewe kwa wenyewe kama pia juu ya msumari wake, na vile vile inalizunguka jua. Na yote hayo ni dalili ya uwezo wa Mwenye kuumba katika kuanzisha uumbaji. Ujuzi wa mambo hayo wakati wa Mtume s.a.w. haukuwepo. Na hii ni dalili nyengine ya kwamba haya hayakuwa ila ni wahyi, ufunuo, ulio toka kwa Mwenyezi Mungu kumpa Mtume s.a.w.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (6) Capítulo: Sura Yunus
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar