Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (28) Capítulo: Sura Al-Nahl
ٱلَّذِينَ تَتَوَفَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ ظَالِمِيٓ أَنفُسِهِمۡۖ فَأَلۡقَوُاْ ٱلسَّلَمَ مَا كُنَّا نَعۡمَلُ مِن سُوٓءِۭۚ بَلَىٰٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Ambao Malaika waliwafisha nao wamejidhulumu nafsi zao! Basi watasalimu amri, waseme: Hatukuwa tukifanya uovu wowote. (Wataambiwa): Kwani! Hakika Mwenyezi Mungu anajua sana mliyo kuwa mkiyatenda.
Hizaya itawashukia makafiri walio endelea na ukafiri wao mpaka Malaika walipo watoa roho, nao wamejidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na kutenda maovu, na wakasalimu amri tena baada ya inadi ndefu walipo jua hakika ya makosa yao. Wakasema uwongo kwa jinsi walivyo shituka: Hatukuwa duniani tukifanya maasi yoyote! Malaika na Manabii watawaambia: Hasha! Hakika nyinyi ni waongo, bali mmetenda maasi maovu kabisa! Na Mwenyezi Mungu, Subhanahu, anajua vyema kila dogo na kubwa mlilo kuwa mkilitenda katika dunia yenu. Hakukuleteeni faida yoyote huko kukataa kwenu!
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (28) Capítulo: Sura Al-Nahl
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar