Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (251) Capítulo: Sura Al-Baqara
فَهَزَمُوهُم بِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَقَتَلَ دَاوُۥدُ جَالُوتَ وَءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَعَلَّمَهُۥ مِمَّا يَشَآءُۗ وَلَوۡلَا دَفۡعُ ٱللَّهِ ٱلنَّاسَ بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لَّفَسَدَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
--Kwa idhini ya Mwenyezi Mungu waliwatimua, na Daudi akamuuwa Jaluti, na Mwenyezi Mungu akampa Daudi ufalme na hikima, na akamfundisha aliyo yapenda. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawapambanishi watu kwa watu basi dunia ingeli haribika. Lakini Mwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila juu ya walimwengu wote.
Basi wale Waumini waliwashinda maadui zao kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Daudi, mmoja wa askari wa Taluti, akamwuuwa Jaluti amiri-jeshi wa makafiri. Na Mwenyezi Mungu akampa Daudi utawala baada ya Twaluti. Akampa na unabii na ilimu yenye manufaa, na akamfunza kwa ayapendayo Mwenyezi Mungu. Na huo ndio mwendo wake Mwenyezi Mungu - kuwanusuru wale wanao tenda mema duniani wala hawafanyi ufisadi. Lau kuwa Mwenyezi Mungu hawasalitishi askari wake kupambana na mafisadi kwa ajili ya kuondoa ufisadi wao, na akawasalitisha waovu wenyewe kwa wenyewe, ulimwengu usingeli endelea. Lakini Mwenyezi Mungu ni Mwenye hisani na fadhila daima milele juu ya waja wake.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (251) Capítulo: Sura Al-Baqara
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar