Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (145) Capítulo: Sura Al-An'aam
قُل لَّآ أَجِدُ فِي مَآ أُوحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَىٰ طَاعِمٖ يَطۡعَمُهُۥٓ إِلَّآ أَن يَكُونَ مَيۡتَةً أَوۡ دَمٗا مَّسۡفُوحًا أَوۡ لَحۡمَ خِنزِيرٖ فَإِنَّهُۥ رِجۡسٌ أَوۡ فِسۡقًا أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَإِنَّ رَبَّكَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Sema: Sioni katika yale niliyo funuliwa mimi kitu kilicho harimishwa kwa mlaji kukila isipo kuwa kiwe ni nyamafu, au damu inayo mwagika, au nyama ya nguruwe, kwani hiyo ni uchafu; au kwa upotofu kimechinjwa kwa jina la asiye kuwa Mwenyezi Mungu. Lakini mwenye kushikwa na dharura, bila ya kutamani wala kupita mipaka, basi hakika Mola wako Mlezi ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Ewe Nabii! Sema: Hivi sasa sipati katika panapo toka mambo ya kuhalalisha na kuharimisha katika niliyo funuliwa mimi wahyi juu ya chakula kilicho harimishwa kula mlaji, isipo kuwa kitu hicho kiwe ni nyamafu, kimekufa na hakikuchinjwa kwa njia za sharia; au damu inayo tiririka, au nyama ya nguruwe - kwani hivyo vilivyo tajwa vinadhuru, na vichafu, havijuzu kula. Na pia katika vitu vilivyo harimishwa kula vinavyo toka katika itikadi sahihi, kwa kuwa wakati wa kuchinjwa lilitajwa jina lisilo kuwa la Mwenyezi Mungu, kama sanamu au muabudiwa mwenginewe! Juu ya hivyo mwenye kulazimika kwa dharura kula kitu katika hivi vilivyo harimishwa, bila ya kuwa anatafuta utamu tu wa kula, na bila ya kupita mpaka wa ile dharura, basi huyo hana dhambi. Kwa sababu Mola wako Mlezi ni Mwenye kughufiria, na Mwenye kurehemu.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (145) Capítulo: Sura Al-An'aam
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar