Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (31) Capítulo: Sura Al-Tawba
ٱتَّخَذُوٓاْ أَحۡبَارَهُمۡ وَرُهۡبَٰنَهُمۡ أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِ وَٱلۡمَسِيحَ ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُوٓاْ إِلَٰهٗا وَٰحِدٗاۖ لَّآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ سُبۡحَٰنَهُۥ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu, na pia Masihi bin Maryamu. Na wala hawakuamrishwa isipo kuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayo mshirikisha nayo.
Hao Mayahudi na Wakristo wamewafanya makuhani wao na mapadri kuwa ni "Marabi", kama ni miungu, kwa kuwapa madaraka ya kutunga sharia, na kuwa maneno yao ndiyo dini, ijapo kuwa yanakhitalifiana na kauli za Mtume wao. Wanawafuata katika upotovu wao, na wakamuabudu Masihi mwana wa Maryamu! Na Mwenyezi Mungu amewaamrisha katika hivyo hivyo Vitabu vyao kwa ndimi za Mitume wao, kuwa wasimuabudu ila Mungu Mmoja, kwa kuwa Yeye hapana anaye stahiki kuabudiwa kwa mujibu wa hukumu ya sharia na akili ila Mungu Mmoja. Mwenyezi Mungu ametakasika na kushirikishwa katika ibada, uumbaji, na sifa.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (31) Capítulo: Sura Al-Tawba
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar